Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

ALAIN TRAORE ATOKA BENCHI NA KUIOKOA BURKINA FASO

 Alain Traore(katikati) akishangilia na wenzake baada ya kuisawazishia timu yake bao katika mechi iliyoisha kwa sare Nigeria 1-1 Burkina Faso (picha na Daily Mail)
  Vincent Enyeama golikipa wa Nigeria alishindwa kuzuia mpira uliopigwa na Alain Traore na kubaki akilalama kwa kushika nyasi tupu.(Picha na Daily Mail)
 Ahmed Musa(kushoto) akimtoka mchezaji wa Burkina Faso katika mechi ilyotawaliwa na Nigeria.(Picha na Daily Mail)
 Emmanuel Emenike akishangilia baada ya kuifungia Nigeria bao huku akiwaacha golikipa na beki wa Burkina Faso wakiwa hawaamini macho yao.(Picha na Daily Mail)
Shabiki wa Timu ya Taifa ya Burkina Faso akiwa amejipamba na kupendeza vilivyo katika pambano na Nigeria.
.............
Nigeria imeanza kampeini yake ya kinyang'anyiro cha kuwania kombe la Mataifa ya Afrika, nchini Afrika Kusini kwa kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja na Burkina Faso katika mechi yao ya ufunguzi ya kundi C.
Nigeria ilipata bao hilo muhimu na la ushindi kupitia kwa msahmbulizi wake Emmanuel Emenike, anayeichezea klabu ya Spartak Moscow ya Urussi kunako dakika ya 23.
Kikosi hicho cha Super Eagles, kilifanya mashambulizi kadhaa katika lango la Burkina Faso, lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda.
Baada ya dakika za kwanza 45, zilimalizika huku Nigeria ikiwa kifua mbele kwa bao moja kwa bila.
Awali Nahodha wa Nigeria Joseph Yobo alisema kushinda kombe hilo sio kazi rahisi, ila wamejitolea kucheza kadri ya uwezo wao, kuhakikisha kuwa Nigeria, inaibuka mshindi.

Amesema dhamira yao kuu, ni kufikiria hatua za robo na nusu fainali.
Mcheza kiungo, Victor Moses ambaye anaiakilisha Nigeria kwa mara ya kwanza naye anasema wamejianda vyema na ana matarajio makubwa kuwa watafanya vyema katika mashindano ya mwaka huu.
Matumaini ya kocha wa Super Eagles, Stephen Keshi, ambaye anaiongoza timu kwa mara ya kwanza katika fainali hizo ya kuandikisha ushindi wake wa kwanza ulitumbukia nyongo pale Burkina Faso iliposawazisha katika dakika za ziada.
Timu zote katika kundi hilo, Ethiopia, Burkina Faso, Nigeria na Zambia sasa zina alama moja kila mmoja.
Nigeria sasa itachuana na Zambia katika mechi yao ijayo kisha icheza na Ethiopia mechi yao ya mwisho ya makundi.
Burkina Faso nayo imeratibiwa kucheza na Ethiopia mechi ijayo kisha ikamilishe kampeinin yake ya raundi ya kwanza na Zambia.

HABARI NA BBC SWAHILI
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top