
Brigitte ambaye nyota yake katika mashindano hayo ya urembo nchini
ilianza kung’aa tangu Kitongoji cha Sinza baada ya kutwaa taji la Sinza
na Baade kutwaa Taji la Redds Miss Kinondoni amedhihirisha ukali wake
baada ya kuwabwaga warembo wenzake 29 waliokuwa wakiwania taji hilo
kutoka Kanda mbambali.
Mshindi
wa Taji la Redds Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred (katikati)
akipunga mkono kwa furaha katika picha ya pamoja na mshindi wa Pili,
Eugene Fabian (kushoto) na Mshindi wa Tatu, Edda Sylvester mara baada ya
warembo hao kutangazwa kuwa washindi wa shindano hilo. Brigitte
anatokea Kitongoji cha Sinza na Kanda ya Kinondoni wakati, Eugene
anatoka Mkoa wa Mara na Kanda ya Ziwa huku Edda ni Miss Kigamboni na
Kanda ya Temeke.
Warembo waliofanikiwa kuingia hatu5 bora ya Redds Miss Tanzania 2012,
kutoka kushoto ni Brigitte Alfred, Eugen Fabian, Happyness Daniel, Edda
Sylvester na Magdalene Roy wakipozi kwa picha.
Post a Comment