Kikosi cha Simba kimehamia mji wa Unguja ambako mchezowa nusu fainali
kombe la mapinduzi dhidi ya AzamFC utapigwa. Simba imepeleka wachezaji
wake wote muhimu
kuelekea mchezo wake na Azam utakaopigwa
hapo kesho saa 2:15 usiku kwenye dimba la Amaan. Hizi ni baadhi ya picha
za wachezaji wakiendelea na mazoezi makali kuelekea mchezo huo.
Kikosi cha Jurgen Klopp kinafanya vizuri lakini wiki hii kitaanza kupata wakati mgumu kwenye safari yao ya kuwani ubingwa tofauti na timu za Manchester United,Man City,Arsenal,Chelsea na Tottenham Hottspur.
Baada ya michuano ya UEFA Nations League kuisha wiki hii zinaingia wiki tatu mfululizo kuelekea Oktoba kabla ya wiki ya mapumziko kwa ajili ya mechi za kirafiki za kimataifa.
Katika vinara wa EPL wanaowania ubingwa wenye ratiba ngumu ni Liverpool.Hebu tuangalia kila timu ratiba yake ilivyo .
LIVERPOOL
Ina kazi ngumu,hilo halina ubishi.Hiki ndio kipindi kinachosemwa ya kwamba ni kipimo kwa klabu hiyo kama kweli ina ubavu wa kuwani Ubingwa itakapoikabili Tottenham Hotspur, Chelsea na Manchester City.
Ugumu umekuja pale ambapo imejikuta ina ratiba ngumu ya EPL lakini ikajikuta inaanza UEFA na Paris Saint-Germain na kuifuata Napoli , wakati huo ikiikaribisha Chelsea katika Carabao Cup.
Lakini pia ikiwa na mechi nyumbani na Southampton, ambapo Liverpool ilishinda mara moja katika mechi nne walizokutana pale Anfield pale timu hizo zilipokutana.
Hapo Jurgen Klopp kwa mara ya kwanza itabidi aanze kupumzisha baadhi ya wachezaji na kuanzisha wengine ili kikosi chake kiweze vuka salama katika kipindi hiki.
Hizi ndio mechi za Liverpool ambazo zinaweza kuipa picha nyingine kabisa msimu huu ambapo itaanza Sep 15: Tottenham (A), Sep 18: PSG (H) (Champions League), Sep 22: Southampton (H), Sep 25/26: Chelsea (H) (Carabao Cup), Sep 29: Chelsea (A), Oct 3: Napoli (A) (CL), na kumaliza Oct 7: Man City (H).
Manchester City
Wakiwa wameanza vizuri dhidi Arsenal, inatazamiwa City watakuwa wameshinda mechi saba dhidi ya saba watakopokuja kumenyana na Liverpool mwezi Oktoba.
Hakuna ubishi, City ana ratiba nyepesi ya EPL, UEFA pamoja na Carabao Cup.
Mechi za City Sep 15: Fulham (H), Sep 19: Lyon (H) (CL), Sep 22: Cardiff (A), Sep 25: Oxford (A) (CC), Sep 29: Brighton (H), Oct 2: Hoffenheim (A) (CL), kabla ya kupepetana Oct 7: Liverpool (H).
Tottenham Hotspur
Tottenham wamepangiwa ratiba ngumu ya Champions League kuliko Liverpool, kwa kuangalia mechi zao mbili za mwanzo kwenye grupu lake.
Carabao Cup droo nayo imekuwa rahisi kwake dhidi ya Lilywhites, ukichukulia mechi hiyo kupigwa pale MK Dons.
Lakini mechi yao ya wikiendi hii dhidi ya Liverpool, EPL itatoa nafasi kwa kocha Mauricio Pochettino kukibadilisha kikosi chake
Spur itaanza wikiendi tarehe Sep 15: Liverpool (H), Sep 18: Inter Milan (A) (CL), Sep 22: Brighton (A), Sep 26: Watford (H) (CC), Sep 29:Huddersfield (A), Oct 3: Barcelona (H) (CL), Oct 6: Cardiff (H).
Manchester United
Jose Mourinho alirekodiwa akianguka pale Wembley siku ya jumamosi imejidhihirisha vivyo hivyo kwa United ambayo imejikuta ikiangukia pua kwenye mechi za mwanzo wa msimu.
Vipigo viwili vimeifanya United ikifanya vibaya na kuzusha gumzo kubwa dhidi yake na wachezaji mahiri klabuni hapo.Hivyo kipindi hiki ndicho muafaka kuinua morali ndani na nje ya klabu hiyo.
Siku ya jumamosi inafunga safari kuifuata Watford kibarua inachotakiwa kukimaliza vizuri ili kuiona United ikipanda nafasi zaidi katika EPL.
Tarehe Sep 15: Watford (A), Sep 19: Young Boys (A) (CL), Sep 22: Wolves (H), Sep 25: Derby (H) (CC), Sep 29: West Ham (A), Oct 2: Valencia (H) (CL), Oct 6: Newcastle (H).
Chelsea
Kama Liverpool, vijana wa London wameanza kwa ushindi wa 100% EPL msimu huu.
Na wana mechi mbili dhidi ya Liverpool katika mechi zijazo ambazo ni moja ya EPL na Carabao Cup ambazo inabidi ifanye vizuri katika kampeni ya kuwa na msimu mzuri.
Swali moja linabakia ni namna gani wataweza kuhimili kucheza alhamisi Europa Ligi na Jumapili EPL na ni namna gani Kocha Maurizio Sarri anayachukulia haya mashindano.
Wikiendi hii Sep 15: Cardiff (H), Sep 20: PAOK Salonika (A) (CL), Sep 23: West Ham (A), Sep 25/26: Liverpool (A) (CC), Sep 29: Liverpool (H), Oct 4: MOL Vidi (A) (EL), Oct 7: Southampton (A).
Arsenal
The Gunners kama wanavyojulikana walianza na mechi ngumu dhidi ya City na Chelsea, lakini toka hapo wameanza kubadilika.
Mechi zao zote za EPL zitakuwa ni zile zilizo songana sana kipindi hiki.
Japokuwa, Arsenal wamepata nafuu kwenye droo ya Europa League ukweli ukiwa watacheza London mara moja siku ya jumamosi dhdi ya Tyneside.
Cristiano Ronaldo, Luka Modric na Mohamed Salah ndio wachezaji watatu wa mwisho ambao watawania tuzo la mchezaji bora wa Fifa mwaka 2018.
Tuzo hizo zinafanyika huku mshambuliaji wa Barcelona raia wa Argentina Lionel Messi, mshindi mara tano wa tuzo la Ballon d'Or amekosa kuorodheshwa katika tatu bora.
Pia hakuna mchezaji yeyote aliyekuwa kwenye kikosi cha Ufaransa kilichoshinda Kombe la Dunia.
Huku winga mreno Ronaldo ambaye ni mshindi wa mwaka 2016 na 2017, alishinda kombe la tano la ligi ya mabingwa na Real Madrid mwezi Mei kabla ya kujiunga na Juventus kwa pauni milioni 99.2.
Kiungo wa kati wa Real Madrid Luka Modric alitajwa kuwa mchezaji bora kwenye Kombe la Dunia mwaka 2018 wakati Croatia ilifika fainali dhidi ya Ufaransa.
Mo Salah anakuwa mchezaji wa kwanza wa EPL kuorodheshwa kwenye tuzo hizo kwa mara ya kwanza toka mwaka 2008, pale Cristiano Ronaldo aliposhinda. Pia ni mchezaji wa kwanza toka bara la Afrika kufika hatua hiyo ya tatu bora toka Samuel Eto'o alipojumuishwa mwaka 2005.
Mmisri Mo Salah alifunga mabao 44 huku Liverpooll ikifika fainali ya ligi ya mabingwa na kushindwa na Real Madrid.
Modric aliwashinda Ronaldo na Salah kwa kushinda tuzo la mwanamume bora wa mwaka wa Uefa wiki iliyopita.
Mshambuliaji wa England Harry Kane ambaye alishinda kiatu cha dhahabu kwenye Kombe la Dunia alikuwa kwenye orodha ya kumi bora lakini amekosa.
Didier Deschamps, ambaye aliiongoza Ufaransa, ameteuliwa kuwania tuzo la kocha wa mwaka, akiwemo raia wa Croatia Zlatko Dalic na meneja wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane.
Tuzo hizo ni kando la Ballon d'Or, baada ya shirikisho la kandanda duniani kukata uhusiano wake na tuzo hilo mwaka 2016.
Jopo la wataalamu wa Fifa waliunda orodha ya wachezaji 10 kwa kila tuzo huku manahodha wa timu za taifa, waandishi wa habari na mashabiki wakimchagua mshindi kila kundi likiwa na asilimia 25 ya kura.
Ni wachezaji nane(8) wa EPL ambao wamewahi kushiriki tuzo za mchezaji bora wa FIFA katika historia ambao ni – Lineker, Shearer, Bergkamp, Beckham, Henry, Lampard, Ronaldo, Torres.
Wachezaji wawili 2 waafrika ambao ni – Weah and Eto'o. Weah akishinda tuzo hiyo mwaka 1995, na Ronaldo mwaka 2008.
Washindi watatangazwa tarehe 24 Septemba huko Royal Festivan mjini London
Jumatano 19 September Kundi E: Ajax v AEK Athens (18.55CET), Benfica v Bayern MΓΌnchen Kundi F: Shakhtar v Hoffenheim (18.55CET), Manchester City v Lyon Kundi G: Real Madrid v Roma, Viktoria Plzen v CSKA Moskva Kundi H: Young Boys v Manchester United, Valencia v Juventus
Mechi kali zinatazamiwa kuwa
Jumatano 3 October: Tottenham v Barcelona Jumanne 23 October: Manchester United v Juventus Jumanne 6 November: Inter v Barcelona Jumatano 28 November: Paris v Liverpool Jumatano 12 December: Ajax v Bayern MΓΌnchen
Kuelekea Fainali Madrid
18/19 September: group stage, matchday one 2/3 October: group stage, matchday two 23/24 October: group stage, matchday three 6/7 November: group stage, matchday four 27/28 November: group stage, matchday five 11/12 December: group stage, matchday six
17 December: Hatua ya 16 bora droo
12/13/19/20 February: round of 16 first leg 5/6/12/13 March: round of 16 second leg
15 March: robo-final na nusu -final droo
9/10 April: Quarter-finals, first leg 16/17 April: Quarter-finals, second leg
30 April/1 May: Semi-finals, first leg 7/8 May: Semi-finals, second leg
Manchester City, Manchester United, Tottenham na Liverpool leo zitajua timu watakazo kabiliana nazo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya katika hatua ya makundi yatakayopangwa leo jioni Alhamisi.
Makundi hayo yatapangwa leo Alhamisi katika mji wa Monaco.
Kumepangwa kuwa na makapu manne yenye timu nane, ambapo kila timu kutoka kila kapu itaunda Kundi,lakini kwa timu zinazotoka nchi moja haziwezi kuwa kundi moja.
Mabingwa wa EPL Man City,waliotolewa na Liverpool katika hatua ya robo fainali msimu uliopita, wako kapu la kwanza na mabingwa watetezi Real Madrid, Mabingwa wa Europa Ligi Atletico Madrid, Barcelona, Bayern Munich, Juventus, Paris Saint-Germain na Lokomotiv Moscow.
Man United na Spurs, waliotolewa kwenye hatua ya 16 bora msimu wa 2017/2018,wako kapu la pili,lenye timu za Borussia Dortmund, Porto, Shakhtar Donetsk, Benfica, Napoli na Roma.
Kikosi cha Jurgen Klopp’s Liverpool watakuwa kapu la tatu na Schalke, Lyon, Monaco, Ajax, CSKA Moscow, Valencia na PSV Eindhoven.
Mabingwa nchini Serbian Red Star, bingwa 1991, atakuwa Viktoria Plzen, Club Brugge, Galatasaray, Young Boys, Inter Milan, Hoffenheim na AEK Athens.
Mechi za mwanzo za makundi zitaanza kati ya Septemba 18 na 19, huku fainali itapigwa katika uwanja wa nyumban wa Atletico Madrid’s Wanda Metropolitano Stadium mnamo June 1.