Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

JE UNAHITAJI PASSPORT ? HIVI NDIYO JINSI YA PATA PASSPORT YAKO YA TANZANIA


Je wajua kuwa sasa unaweza ingia Sauzi bila kuwa na Visa? Yes ni kweli kabisa unaweza ingia Sauzi bila kuomba visa. Unachotakiwa tuu ni kuwa na Passport yako ya Tanzania, hapa nazungumzia Passport ya kimataifa kama hiyo pichani hapo juu.
Bila shaka unafahamu kuwa kwa nchi za Afrika mashariki si lazima uwe na hiyo Passport ya kimataifa, kuna Passport maalum za Afrika Mashariki. Ila leo tuzungumzie namna ya kupata hiyo Passport ya kimataifa.

Bei: 
Kwa mujibu wa website ya uhamiaji immigration.go.tz, ni kuwa utahitaji kulipia Tshs. Elfu Hamsini. Malipo haya yanalipwa hivi: Elfu KUMI wakati wa kuchukua fomu, halafu ukirudisha fomu unalipia ElFU AROBAINI.

Masharti : 
Inakupasa uwe na cheti cha kuzaliwa, na pia uwe na cheti cha kuzaliwa cha mmoja wapo wa mzazi wako. Kama mzazi hana cheti basi atahitaji kupata kiapo cha mahakamani kuthibitisha kuwa ni mtanzania. Kiapo hicho huitwa Affidavit.
Pia unahitaji kuwa na picha TANO za kiwango maalum cha Passport size, maelezo ya namna ya kupiga picha hizi zinazohitaji utayapata kwa ofisi ya uhamiaji utakayoenda kuomba Passport. Ushauri kwako, usijipigie tuu picha ukaziwasilisha uhamiaji, hakikisha unawasiliana na ofisi ya uhamiaji nao watakupa maelekezo sahihi kuhusu picha wanazotaka.

Fomu ya maombi:  
Utatakiwa uende ofisi ya uhamiaji na kulipia fomu maalum ya maombi. Wewe utajaza hiyo fomu ambayo pamoja na mambo mengine itakuwa na sehemu maalum ya mdhamini wako kujaza na kutia saini. Wewe utatakiwa kutia saini mbele ya ofisa wa uhamiaji siku ya kuirudisha fomu husika.

Mahitaji mengine: 
Utahitajika kuwa na sababu maalum ya kwanini unataka kusafiri kwenda nje ya nchi. Uthibitisho maalum unahitajika, mfano barua ya mwaliko wa kumtembelea mtu aliyepo nje ya nchi, au barua ya kuitwa kufanya kazi nje ya nchi, au barua ya kukubaliwa kujiunga na chuo nje ya nchi, uthibitisho wa tiketi ya kurudi toka nchi unayotaka kutembelea kibiashara, au uthibitisho mwingine kama wa safari ya matibabu, au michezo.


Inachuku muda mpaka kupata Passport?: 
Inategemea, ila kwa kawaida si zaidi ya wiki mbili toka uwasilishe fomu kamili na kutimiza masharti yote.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

1 comments:

Natakiwa kuonesha bank statement kwa afisa uhamiaji?

Reply

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top