Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CHADEMA YAIBUKA NA MITAA 6,CCM WAAMBULIA 3 UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA USA RIVER-ARUSHA

DSCN6121Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari akiwa kwenye gari ya wazi na wafuasi wa Chadema katika mji wa Usa River wakifurahia matokeo ya uchaguzi kuwatafuta wenyeviti wa Serikali za mitaa ambapo Chadema waliweza kuibuka kidedea kwa kujinyakulia uongozi wa mitaa 6 kati ya tisa iliyokuwa inagombaniwa.
DSCN6120
DSCN6126
DSCN6123Shamrashamra za kushangilia ushindi
DSCN6101Mh Joshua Nassari akipokea matokeo ya awali kutoka vituo mbalimbali vya kupigia kura ndani ya Halmashauri ya mji mdogo wa Usa River kwa njia ya simu ndani ya kituo cha chama chake cha kufanya majumuisho ya kura kwa upande wa Chadema jana.
DSCN6103Hali ya barabara ilikuwa ni ya utelezi na matope sana kwa meoneo mengi ya mji
DSCN6110Mh Nassari akifurahia matokeo yaliyokipatia ushindi chama chake na baadhi ya viongozi wa chama na wadau wengine mahali walipojibanza barazani kukwepa mvua
DSCN6116Hapa Nassari alikuwa akiwafahamisha wananchi matokeo rasmi ya uchaguzi ambao walishiriki, baada ya kupata matokeo ya maeneo yote.
DSCN6100Gari iliyotolewa na mmoja wa madiwani wa Chadema mjini Arusha ili kusaidia kampeni hizo zilizopelekea CHADEMA kuipiga kumbo CCM
DSCN6104Kabla ya matokeo ya jumla, CCM nao walionekana mitaani wakipita kwa shamrashamra kuanza kushangilia lakini furaha yao ilizimwa ghafla na matokeo ya mwisho baada ya kujikuta wameambulia mitaa 3 tu kati ya 9.

 Katika uchaguzi huo uliofanyika jana huku mvua kubwa ikinyesha maeneo tofauti kiasi cha kuharibu mawasiliano kwa baadhi ya maeneo, ulishirikisha jumla ya vyama vitatu ambavyo ni CHADEMA, CCM na AFP ambao walishiriki mitaa miwili tu.
 
Kwa matokeo hayo ya viti sita kwenda CHADEMA, ni wazi kuwa nafasi ya kuongoza Halmashauri ya Mji mdogo wa Usa River itachukuliwa na chama hicho kwa maana kwamba tayari wanakura nyingi endapo kila chama kitapigia upande wake! Viti maalumu pia vinaweza kuongeza idadi ya kura za Chadema katika kumchagua meya wa Halmashauri ya Mji huo mdogo wa Usa River.

Chadema waliibuka washindi kwa kuchukua uenyekiti wa mitaa ya Mji Mwema, Kisambale, Manayata Kati na Banana.

Mitaa mingine ni Magadini na Ngarasero ambao ulielezwa kuwa ngome kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM katika mji huo.

CCM kwa upande wao waliweza kujinyakulia mitaa ya Mlima Sioni, Magadirisho na Usa Madukani.

Chanzo Noise of Silence Blog.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top