Kocha
 Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 21 
kitakachoingia kambini Jumapili (Februari 3 mwaka huu) kwa ajili ya 
mechi ya kirafiki dhidi ya Cameroon (Indomitable Lions).
Akizungumza
 na Waandishi wa Habari, Dar es Salaam leo (Januari 31 mwaka huu), Kim 
amesema mechi dhidi ya Cameroon itakuwa kipimo kizuri kwake kwa sababu 
ni sehemu ya maandalizi kabla ya kucheza mechi ya mchujo ya Kombe la 
Dunia dhidi ya Morocco itakayofanyika Machi mwaka huu.
“Itakuwa
 mechi ngumu na kipimo sahihi kwetu. Tuko tayari, tutacheza kwa staili 
yetu kwa sababu ni sehemu ya maandalizi kabla ya mechi dhidi ya Morocco.
 Ni mechi nzuri kwa sababu wachezaji wameonyesha wako tayari.
“Tumetoka
 kucheza dhidi ya Zambia na Ethiopia. Lengo ni Taifa Stars kucheza 
fainali za AFCON 2015, kwa hiyo mechi dhidi ya Cameroon ni sehemu ya 
mipango yetu kuhakikisha tunafika huko,” amesema Kim ambaye amerejea 
nchini juzi kutoka Afrika Kusini kuzifuatilia timu za Morocco na Ivory 
Coast zilizo kundi moja na Tanzania katika mechi za mchujo za Kombe la 
Dunia.
Taifa
 Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na Morocco, 
Machi 24 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Stars inashika nafasi
 ya pili katika kundi lake nyuma ya Ivory Coast inayoongoza. Timu 
nyingine katika kundi hilo ni Gambia.
Wachezaji
 aliowaita kwenye kikosi chake ni makipa Juma Kaseja (Simba), Mwadini 
Ali (Azam) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), 
Nassoro Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Nadir Haroub (Yanga), 
Kelvin Yondani (Yanga), Shomari Kapombe (Simba) na Issa Rashid (Mtibwa 
Sugar).
Viungo
 ni Amri Kiemba (Simba), Simon Msuva (Yanga), Frank Domayo (Yanga), 
Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Salum Abubakar (Azam), Khamis Mcha (Azam),
 Athuman Idd (Yanga) na Mwinyi Kazimoto (Simba). Washambuliaji ni Mrisho
 Ngasa (Simba), na Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya
 TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Post a Comment