Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

NI HAKI YA MSINGI KABISA WANANCHI WA MKOA WA MTWARA KUANDAMANA KUPINGA GESI KUPELEKWA DAR ES SALAAM.WAKATI HAWAJUI HATIMA YAO.

M'Kiti wa Jumuiya ya Vijana Ya Chama Cha Wananchi-CUF, Leo ameongea na Vyombo vya Habari. Na haya ndio Maelezo ya Press ya Leo.

Jumuiya ya vijana CUF Taifa inaendelea kuunga mkono harakati zinazoendelea mkoani Mtwara za kupinga mpango wa serikali wa kujenga bomba la kusafirishia gesi asilia kutoka mtwara hadi dare s salaam, jumuiya ya vijana CUF taifa inaamini gesi inahamishwa kwa matakwa ya watu Fulani na sio kwa manufaa ya taifa kama inavyoelezwa na serikali, jumuiya haioni sababu ya kiuchumi ya kuhamisha gesi Mtwara kupeleka Dar es salaam au sehemu nyingine yeyote ile kwa kuzingatia yafuatayo:-

1. Uamuzi wa kuhamisha gesi sio wa kiuchumi na haukuzingatia misingi ya kiuchumi kwani kama serikali ingeamua kujenga mitambo ya kufulia gesi (Plants) mkoani Mtwara ingeokoa mabilioni ya pesa yanayotumika kusafirishia gesi asilia toka Mtwara kwenda Dar es Salaam, inasemekana bomba moja la mita tano (5) inagharimu fedha za kitanzania takribani bilioni tatu (3), hii ni hatari tujiulize umbali uliopo kati ya Mtwara na Dar nikilometa ngapi? Kwani ni zaidi ya kilometa 560 mara hiyo bilioni 3 tunazani ni pesa kiasi gani zitatumika kwa ajli ya mradi huo?kwanini wasifanye opportunity cost ya kujenga hizo plants Mtwara? ili kuokoa gharama za usafirishaji wa gesi wanasafirisha na wanaenda kujenga plants nyingine Dar hivi hatuoni Taifa linaingia gharama mara mbili?

2. Ujenzi wa vinu vya kufulia gesi asilia Mtwara utasaidia kuchochea maendeleo ya mikoa ya kusini kwa kuwahakikishia ajira vijana ambao kila siku wanapanga mikakati ya kwenda Dar kutafuta ajira na maisha bora! Lazima Taifa lifanye diversification of economy kwani hata mataifa ya Ulaya na Marekani yalifanikiwa kwa kufanya diversification of economy sio kila mradi tuupeleke Dar es Salaam, tunasababisha population na kufanya uchumi kuwa concentrated in a single area hii ni hatari kwa mipango ya muda mrefu ya taifa hili.

3. Kujengwa kwa mitambo hiyo katika mikoa ya kusini itasaidia kuchochea maendeleo ya miundo mbinu mbalimbali kama barabara, bandari, na reli kwa lazima serikali itajenga miundo mbinu imara kwa ajili ya kusafirisha gesi iliyo tayari kwa kutumiwa na watumiaji mbalimbli kutoka mikoa tofauti tofauti, Taifa linahitaji mawazo yakinifu ya kuwasaidia wananchi wenye kipato cha chini hasa wanaotoka mikoa ya kusini.

Jumuiya ya vijana inashangazwa na kauli tata inayotolewa na viongozi wa Serikali ya CCM kwani ikumbukwe kuwa tarehe 25/07/2011 kwenye maadhimisho ya siku ya mashujaa Rais Kikwete aliwahutubia wananchi wa Mtwara na kuwahakikishia kuwa katika utawala wake atainua mikoa ya kusini kiviwanda na kumtaka Meya wa Manispaa ya Mtwara – Mikindani kutenga maeneo kwa ajili ya wawekezaji, wananchi wanahoji utawala wake unaelekea ukingoni hauna hata dalili ya kiwanda kimoja badala yake kunazoezi la kutaka kuhamisha gesi hiyo na kupelekwa Dar es Salaam, je hivi kweli Rais Kikwete na CCM yake wana mapenzi ya dhati na watu wa kusini?
Jumuiya ya vijana CUF Taifa inaendelea kushangazwa na taarifa ya Waziri wa nishati na madini Mheshimwa Sospeter Muhongo kwa kudai kuwa eti asilimia kumi na nne (14%)tu ya gesi iliyogunduliwa ndiyo inatoka Mtwara, kwanini sasa wasipeleke mradi huo wa bomba la kusafirishia gesi sehemu nyingine badala ya Mtwara? Jumuiya inasisitiza kuwa wanamtwara hawapingi gawio la pato linalotokana na gesi kutumika sehemu nyingine yeyote ya nchi, kwani ikumbukwe kuwa hata kwenye ushuru wa zao la korosho ambalo limekuwa zao la pili kuingizia ushuru wa Taifa mwaka jana wananchi hawajahoji lolote juu gawio la ushuru huo?

Kwa hiyo Jumuiya ya vijana CUF Taifa inashangazwa na kauli ya viongozi wa CCM ya kusema kuwa wanamtwara wanahitaji gesi iwanufaishe wao wakati ukweli ukijulikana kuwa kilio cha wanamtwara nikutaka uwekezwaji unaotokana na gesi ufanywe Mtwara na Lindi kama ilivyofanywa kwenye viwanda vya sukari, kwani miwa inalimwa Tuliani, Mtibwa, na Kilombero – Morogoro na viwanda viko huko kwa nini gesi iwe Mtwara plant iwekwe Dar es Salaam?

Kwa hiyo Jumuiya ya vijana CUF Taifa inaunga mkono gesi kutosafirishwa kupelekwa Dar es Salaam.

Imetolewa na,
Jumuiya ya Vijana CUF Taifa,
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top