Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

YANGA YAENDELEA NA MAZOEZI



Kikosi cha timu ya Young Africans Sports Club leo kimeanza tena mazoezi baada ya kuwa na mapumziko ya siku mbili kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka katika uwanja wa mabatini Kijitonyama, kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya timu ya JKT Oljoro kutoka jijini Arusha mchezo utakaofanyika Aprili 10 2013.
Young Africans ambayo mwishoni mwa wiki ilitoka suluhu ya bila kufungana na timu ya Polisi Morogoro, bado inaendelea kuongoza msimamo wa Ligi Kuu kwa kuwa na poniti 49, zikiwa ni pinti sita (6) mbele ya timu ya Azam FC inayoshika nafasi ya pili ikiwa na pointi 43.
Katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Jamhuri mjiji Morogoro, ulikosa radha kutokana na waamuzi kutokua makini na kutofautiana katika maaamuzi mbali mbali hali iliyopelekea mchezo kuishia kwa sare ya tasa 0-0.
Baada ya suluhu ya jumamosi kikosi cha Yanga kimeanza mazoezi leo asubuhi kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya timu ya JKT Oljoro ambayo katika mchezo wa awali uliofanyika jijini Arusha, watoto wa jangwani waliibuka na ushindi wa bao 1-0, bao lililofungwa na mlinzi Mbuyu Twitew.
Yanga imebakisha jumla ya michezo mitano (5) ili kukamilisha michezo ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom 2012/2013, michezo iliyobaki ni kama ifuatavyo:
Aprili 10, 2013 : Young Africans Vs JKT Oljoro (Uwanja wa Taifa - Dar es salaam)
Aprili 13, 2013 : Mgambo Shooting Vs Young Africans (Mkwakwani - Tanga)
Aprili 21, 2013 : JKT Ruvu Stars Vs Young Africans (Uwanja wa Taifa - Dar es salaam)
May 01, 2013  : Young Africans Vs Coastal Union (Uwanja wa Taifa - Dar es salaam)
May 18, 2013 : Simba SC Vs Young Africans (Uwanja wa Taifa - Dar es salaam)
Wachezaji waliofanya mazoezi leo ni :
Walinda mlango: Ally Mustafa 'Barthez' na Yusuph Abdul
Walinzi: Shadrack Nsajigwa, Stephano Mwasika, Oscar Joshua, Juma Abdul, Godfrey Taita, Kelvin Yondani na Nadir Haroub 'Cannavaro'
Viungo: Omega Seme, Salum Telela, Nurdin Bakari, Frank Domayo, Rehani Kibingu, David Luhende na Haruna Niyonzima
Washambuliaji: Said Bahanuzi, Saimon Msuva, Hamis Kiiza, George Banda, Nizar Khalfani na Didier Kavumbagu 
Wachezaji ambao hawakuweza kushiriki katika mazoezi ya leo ni mlinda mlango Said Mohamed na Jerson Tegete ni majeruhi, Athuman Idd 'Chuji' anayeumwa tonses na mlinzi Mbuyu Twite ambaye anauguliwa na mkewe.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top