Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CHADEMA KUPINGA MAHAKAMANI USHINDI WA SIMBACHAWENE,LUBELEJE

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilaya ya Mpwapwa, mkoani Dodoma, kinapanga kwenda mahakamani kupinga matokeo ya ubunge na udiwani kwa baadhi ya kata katika majimbo ya Mpwapwa na Kibakwe, kwa madai kuwa uchaguzi uligubikwa na rushwa na ukiukwaji wa taratibu na sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Katibu wa Chadema wilayani humo, Fabian Moke, alisema kutokana na hali hiyo chama hicho kinajiandaa.

kwenda mahakamani kupinga matokeo hayo. Alisema kufuatia kasoro hizo, wagombea wote wa chama hicho katika maeneo hayo waligoma kusaini matokeo kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa uchaguzi. “Tumeitisha kikao cha dharura cha viongozi ngazi ya wilaya na jimbo ili kueleza hali hiyo ya sintofahamu kwa wanachama wetu,” alisema Moke.

Hata hivyo, msimamizi wa uchaguzi wilayani humo, Mohamed Maje, alisema sheria ya uchaguzi haikatazi kutangaza matokeo hata kama mgombea kagoma kusaini, bali anachotakiwa kufanya mgombea huyo ni kufuata taratibu za kisheria kutafuta haki yake.

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu, George Lubeleje (CCM) aliibuka mshindi wa nafasi ya ubunge Jimbo la Mpwapwa kwa kupata kura 32,208 sawa na asilimia 74.46, huku nafasi ya udiwani CCM ikishinda kata zote 15.

Kwa upande wa Jimbo la Kibakwe, George Simbachawene (CCM) ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini, alitangazwa mshindi wa nafasi hiyo kwa kupata kura 37,327 sawa na asilimia 81, huku kwenye udiwani CCM kikishinda viti vyote 18.

CHANZO: NIPASHE
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top