Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.
Waziri
Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa
kadhaa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi baada ya
kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo
hakuyafurahia.
Maafisa
hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze
kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.
Katika
Ziara hiyo ya ghafla Waziri mkuu Kasim Majaliwa awasimamisha kazi
kamishna wa kodi Tiagi Masamaki na Habibu Mpozya kitengo cha huduma kwa
wateja kutokana ubadhilifu wa fedha kwa makontena zaidi ya 300
yaliyopotea.
Wengine ni Haruni Mpande -ICT, Hamisi Ali Omari na Eliachi Mrema incharge wa ICD na amemuru wrote wakamatwe uchunguzi uendelee.
Walohamishwa kituo na kupelekwa mikoani ni Nsajigwa Mwandege, Robert Nyoni na Anangisye Mtafya
Maofisa
hao wametakiwa kusalimisha hati zao za kusafiria hii imekuja baada ya
kubainika kuwa makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya tsh bilioni 80
hayaonekani katika mtandao wa TRA huku data za mamlaka ya bandari
yanataarifa
Post a Comment