Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

PROFESA BAREGU AMTAHADHARISHA MAGUFULI KUHUSU WATU BINAFSI KUCHANGIA MICHANGO KWENYE HAFLA ZA BUNGE


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA), Profesa Mwesiga Baregu amesema anatilia shaka hatua ya Taasisi muhimu kama Bunge kukusanya michango kutoka kwa Taasisi za umma ili kuendeshea shughuli zake, ikiwamo hafla ya uzinduzi wa Bunge mjini Dodoma.

Aidha, Profesa Baregu ameshangazwa na hatua ya Rais John Magufuli kupokea fedha hizo na kuzibariki kutumika katika kununulia vitanda katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili bila kuhoji malengo na msingi wa mhimili huo wa kutunga sheria kuchangiwa fedha hatua ambayo msomi huyo amedai kuwa ni kumwingiza Rais kwenye mtego wa ufisadi wa kimfumo.

“Bunge ni taasisi nyeti sana kuruhusu kuchangiwa pesa na watu au taasisi ambazo linapaswa kuzisimamia. Mara kadhaa wakuu wa mashirika haya hutakiwa kuhojiwa ikiwemo kuwasilisha matumizi yao mbele ya Kamati za Bunge; Je, kweli Bunge litakuwa na nguvu ya kuzisimamia endapo linapokea michango kutoka kwenye Taasisi hizo?” amehoji Profesa Baregu.

Profesa Baregu ameelezea kitendo cha Bunge kukusanya michango kwa ajili ya hafla kuwa ni ufisadi wa kimfumo ambao haustahili kuvumiliwa.
 
Aidha msomi huyo amesema anategemea kuwa kwa umakini alionao Rais Magufuli hatalifimbia macho hili na atawataka Bunge wajieleze ni kwa namna gani wameingia kwenye ufisadi huu wa mfumo na ikiwezekana kuwachukulia hatua wote waliohusika.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top