STAA wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford amewataka
wasanii wenzake waliotofautiana wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu
uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu kumaliza bifu kwani zoezi hilo
limemalizika na maisha lazima yaendelee.
kipiga stori na gazeti hili, Shamsa alisema anamshukuru Mungu yeye
hakuwa na bifu na mtu kwa sababu alijua kabisa kuna maisha baada ya
uchaguzi ila wenzake waliingia katika migogoro ya kisiasa kwa tofauti za
kiitikadi.
“Jamani wasanii wenzangu mliotofautiana na kuwekeana bifu kipindi cha
uchaguzi, nawasihi mmalize ili tufanye kazi kwa bidii kwani wakati wote
wa kampeni tasnia ya filamu ilikuwa imelala,mimi nimeshaanza kwa kasi
ya ajabu na hivi karibuni filamu yangu mpya itakuwa mtaani,” alisema
Post a Comment