Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TGDC YATARAJIA KUZALISHA UMEME MEGAWATI 200 IFIKAPO 2020.

 Meneja Mkuu wa Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe akichangia mada wakati wa Warsha ya siku mbili inayofanyika Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia.
 Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo ya Biashara wa Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Bwana Kato Kabaka akitoa mada wakati wa Warsha ya siku mbili inayofanyika Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia.
 Mtaalamu wa masuala ya nishati toka Benki Kuu ya Dunia (ESMAP) Bwana Thrainn Fridriksson (aliyesimama mbele) akitoa mada wakati wa Warsha ya siku mbili inayofanyika Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia.
 Mtaalam wa masuala ya nishati ya jotoardhi toka Shirika la Pertamina Geothermal Energy la nchini Indonesia Bwana Hendrik Kurniawan Sinaga (kulia) akitoa mada wakati wa Warsha ya siku mbili inayofanyika Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia. Kuhsoto ni Mtaalam mwenzie wa masuala hayo Bwana Agus Zuhro.
 Wadau mbalimbali wa masuala ya nishati ya jotoardhi wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wakati wa Warsha ya siku mbili inayofanyika Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia.
Wadau mbalimbali wa masuala ya nishati ya jotoardhi wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya Warsha Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia.
Picha zote na Benedict Liwenga, Maelezo.

Na Benedict Liwenga, Maelezo.
TGDC imepewa lengo na Serikali la kuhakikisha kuwa inazalisha umeme wa Megawati 200 na kuuingiza katika gridi ya Taifa kufikia mwaka 2020.

Kauli hiyo imetolewa jana na Meneja Mkuu wa Shirika la Uendelezaji Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC) Mhandisi Boniface Njombe wakati wa warsha ya siku mbili iliyofanyika Jijini Dar es Salaam ambayo iliwakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi.

Mhandisi Njombe alisema kuwa warsha hiyo ina lengo la kujadili njia mbalimbali zilizotumiwa na baadhi ya mashirika hayo hadi kufanikiwa kupata nishati hiyo ikiwemo uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC. 

“Matokeo ya warsha hii tuliyoifanya tumeweza kuwasiliana na wenzetu wa Benki ya Duni (ESMAP) kwa kukusanya wataalam toka taasisi mbalimbali pamoja na Mashirika mbalimbali ambayo yamewahi kufanya kazi hii ya utafutaji wa nishati ya jotoardhi na lengo letu ni kutaka kufahamu njia ambazo wenzetu walizitumia mpaka kufanikiwa ili na sisi tupate kujifunza”, alisema Njombe.

Aidha, aliongeza kuwa warsha hiyo itawezesha rasilimali chache zilizopo ziweze kutumika ipasavyo katika kuleta matokeo ambayo TGDC inatarajia kuyapata ili kuhakikisha kuwa lengo la upatikanaji wa nishati hiyo linafikiwa.

Sambamba na warsha hiyo TGDC kupitia Wizara ya Nishati na Madini wametiliana saini Mkataba wa makubaliano na Shirika linaloshughulikia nishati ya Jotoardhi la nchini Iceland (ICEIDA) utakaoisadia Tanzania kupatiwa vifaa mbalimbali vitakavyotumika katika maeneo ambayo jotoardhi inasadikiwa kupatikana.

Utiaji saini wa mkataba huo ulifanywa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja na kwa upande wa nchi ya Iceland ulifanywa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la ICEIDA Bwana Engilbert Gudmundsson ukushuhudiwa na Meneja Mkuu wa Shirika la Uendelezaji Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC) Mhandisi Boniface Njombe na Wanasheria.

Akiongea mara baada ya utiaji saini wa mkataba huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja alilishukuru shirika la ICEIDA la nchini Iceland kwa mchango wao mkubwa wa kukubali kulisadia shirika la TGDC ili kuhakikisha kuwa nishati hiyo inapatikana.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la ICEIDA Bwana Engilbert Gudmundsson ameahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza nishati hiyo kwa kuendelea kutoa msaada wa kiufundi na vifaa vinavyotumika katika utafutaji na uchimbaji wa nishati hiyo.

Warsha hiyo ilihusisha wadau mbalimbali wakiwemo watu wa Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia kwani hawa wote wameweza kufanikiwa kuipata nishati hiyo, hivyo watatoa mchango mkubwa kuliwezesha shirika la TGDC kupata mafanikio na hatimaye nishati hiyo kuweza kupatikana.

TGDC NI Shirika Tanzu la Tanesco lililoanzishwa Desemba 2013 na kuanza rasmi kufanya kazi zake mwezi Julai 2014 ili kuharakisha upatikanaji wa nishati ya jotoardhi nchini.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top