Arsenal-v-Chelsea (1)
Diego Costa akishangilia ushindi.
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa ameisaidia klabu yake kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila mbele ya wapinzani wao wa kutokea jiji moja la London, Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza, mchezo uliochezwa katika uwanja wa Emirates unaomilikiwa na Arsenal.


Costa alifunga goli hilo katika dakika ya 23 baada ya kuunganisha mpira mrefu uliopigwa na beki wa klabu hiyo, Branislov Ivanovic goli lilidumu kwa dakika zote 90 za mchezo huo hadi mwamuzi Mark Clattenburg anapuliza filimbi ya kumalizika kwa mchezo huo.


Aidha Arsenal ilimaliza mchezo huo ikiwa na wachezaji 10 pekee uwanjani baada ya beki wa timu hiyo, Per Mertesacker kuonyeshwa kadi nyekundu katika dakika 18 ya mchezo huo baada ya kumchezea vibaya mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa.


Baada ya matokeo hayo Arsenal imebaki na alama zake 44 huku ikiwa katika nafasi ya 3 nyuma ya Manchester Citty na Leister City na Chelsea ikipanda kwa nafasi moja kutoka nafas ya 14 hadi 13 huku ikiwa na alama 28.


Matokeo mengine ya Ligi Kuu ya Uingereza iliyochezwa jana Jumapili, Januari 24 ni Everton iliyowakaribisha Swansea City na mchezo huo kumalizika kwa Swansea kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa moja, magoli ya Swansea yakifungwa na Gylfi Sigurdsson dakika ya 17 na Andre Ayew katika dakika ya 34 huku beki wa Swansea Jack Cork akijifunga goli la kufutia machozi kwa Everton katika dakika ya 26.
Diego Costa [blue] akifunga goli
Diego Costa (blue) akifunga goli.
Diego Costa [blue] akimtoka beki wa Arsenal, Hectoe Bellerin [nyekundu] katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza kati ya Arsenal na Chelsea
Diego Costa (blue) akimtoka beki wa Arsenal, Hectoe Bellerin (nyekundu) katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza kati ya Arsenal na Chelsea.
Kiungo wa Arsenal, Mesut Ozil akiwania mpira na Eden Hazard wa Chelsea
Kiungo wa Arsenal, Mesut Ozil akiwania mpira na Eden Hazard wa Chelsea.
Kiungo wa Arsenal, Metheu Flamini [nyekundu] akiwania mpira na kiungo wa Chelsea, William [blue]
Kiungo wa Arsenal, Metheu Flamini (nyekundu) akiwania mpira na kiungo wa Chelsea, William (blue).
Refa wa mchezo huo, Mark Clattenburg akimwonesha Mertesacker kadi nyekundu
Refa wa mchezo huo, Mark Clattenburg akimwonesha Mertesacker kadi nyekundu.
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger akilalamika kwa refa wa mchezo huo, Mark Clattenburg
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger akilalamika kwa refa wa mchezo huo, Mark Clattenburg.
Per Mertesacker akiwa ameketi na Oliver Giroud baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu
Per Mertesacker akiwa ameketi na Oliver Giroud baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.