Diego Costa akishangilia ushindi.
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Mshambuliaji
 wa Chelsea, Diego Costa ameisaidia klabu yake kuibuka na ushindi wa 
goli moja kwa bila mbele ya wapinzani wao wa kutokea jiji moja la 
London, Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza, mchezo 
uliochezwa katika uwanja wa Emirates unaomilikiwa na Arsenal.
Costa
 alifunga goli hilo katika dakika ya 23 baada ya kuunganisha mpira mrefu
 uliopigwa na beki wa klabu hiyo, Branislov Ivanovic goli lilidumu kwa 
dakika zote 90 za mchezo huo hadi mwamuzi Mark Clattenburg anapuliza 
filimbi ya kumalizika kwa mchezo huo.
Aidha
 Arsenal ilimaliza mchezo huo ikiwa na wachezaji 10 pekee uwanjani baada
 ya beki wa timu hiyo, Per Mertesacker kuonyeshwa kadi nyekundu katika 
dakika 18 ya mchezo huo baada ya kumchezea vibaya mshambuliaji wa 
Chelsea, Diego Costa.
Baada
 ya matokeo hayo Arsenal imebaki na alama zake 44 huku ikiwa katika 
nafasi ya 3 nyuma ya Manchester Citty na Leister City na Chelsea 
ikipanda kwa nafasi moja kutoka nafas ya 14 hadi 13 huku ikiwa na alama 
28.
Matokeo
 mengine ya Ligi Kuu ya Uingereza iliyochezwa jana Jumapili, Januari 24 
ni Everton iliyowakaribisha Swansea City na mchezo huo kumalizika kwa 
Swansea kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa moja, magoli ya Swansea 
yakifungwa na Gylfi Sigurdsson dakika ya 17 na Andre Ayew katika dakika 
ya 34 huku beki wa Swansea Jack Cork akijifunga goli la kufutia machozi 
kwa Everton katika dakika ya 26.
Diego Costa (blue) akifunga goli.
Diego
 Costa (blue) akimtoka beki wa Arsenal, Hectoe Bellerin (nyekundu) 
katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza kati ya Arsenal na Chelsea.
Kiungo wa Arsenal, Mesut Ozil akiwania mpira na Eden Hazard wa Chelsea.
Kiungo wa Arsenal, Metheu Flamini (nyekundu) akiwania mpira na kiungo wa Chelsea, William (blue).
Refa wa mchezo huo, Mark Clattenburg akimwonesha Mertesacker kadi nyekundu.
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger akilalamika kwa refa wa mchezo huo, Mark Clattenburg.
Per Mertesacker akiwa ameketi na Oliver Giroud baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment