Siku
chache baada ya kumtimua kazi aliyekua kocha wao mkuu Dylan Kerr
mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu ya simba Zacharia Hans Poppe
amesema hawayumbishwi na lawama za baadhi ya wanachama wao kwa kuwa
wanachohitaji ni kutimiza malengo yao
Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba Zacharia Hans Poppe
Akizungumza
na East Africa Radio Poppe amesema kuwa wameamua kumfuta kazi kocha
huyo baada ya kugundua ameshindwa kuwajenga wachezaji wake tofauti na
ilivyo sasa chini ya kocha Jackson Mayanja.
Poppe amesema walikua wakimshauri kerr juu ya stamina ya wachezaji wao kuwa mbovu lakini hakuwa msikivu hali iliyopelekea kupoteza imani nae.
Katika hatua nyingine Hans Poppe amesema ni jambo la kawaida kwa kocha kushindwa kazi kwenye timu yake hata kama ni bora mfano mzuri ni kwa Jose Mourinho na Luis Van Gaal ambao katika hali ofauti wameshindwa kuonyesha ubora wao ndani ya Chelsea na Manchester united.
Poppe amesema walikua wakimshauri kerr juu ya stamina ya wachezaji wao kuwa mbovu lakini hakuwa msikivu hali iliyopelekea kupoteza imani nae.
Katika hatua nyingine Hans Poppe amesema ni jambo la kawaida kwa kocha kushindwa kazi kwenye timu yake hata kama ni bora mfano mzuri ni kwa Jose Mourinho na Luis Van Gaal ambao katika hali ofauti wameshindwa kuonyesha ubora wao ndani ya Chelsea na Manchester united.
Post a Comment