Mbali na
CAF kutoa agizo kwa vyama vyake vya soka kumuunga mkono Sheikh Salman
bado mgombea huyo alishindwa kufurukuta mbele ya Gianni Infantino ambaye
alishinda kiti hicho cha urais kwa tofauti kubwa ya kura na kuashiria
huenda kuna nchi wanachama wa CAF hawakumpigia kura Sheikh Salmani.
Shaffihdauda.co.tz
imefanya mahojiano maalumu na rais wa TFF Bw. Jamal Malinzi kutaka
kujua hasa ni kitu gani kimemuangusha Sheikh Salman licha ya Afrika bara
lenye kura nyingi kutangaza kumuunga mkono rais huyo wa shirikisho la
soka la Asia.
“Tumepata rais mpya wa FIFA sasa Gianni Infantino
nimeongea na waandishi wa habari wa kimataifa na sasa naongea na Clouds
TV, Clouds FM na shaffihdauda.co.tz ni kwamba tumekubali matokeo ya
uchaguzi, uchaguzi ni uchaguzi kikubwa sasahivi ni kutoa ushirikiano kwa
rais mpya Infantino na kuhakikisha mpira duniani unaendelea na
tunaamini kwa dhati kabisa sasa tumeondoka kwenye hali ya mtikisiko
tuliyokuwanayo baada ya matatizo yaliyotokea chini ya mzee Blatter
Katibu Mkuu wake pamoja na Michel Platini na wengine”.
“Yalitokea
matatizo lakini sasa ule mtikisiko umekwisha sasahivi mpira Afrika
umetulia, Asia umetulia, America umetulia, Ulaya umetulia kwahiyo sasa
tutulie tutengeneze mpira wetu na tunaamini kwa dhati kabisa kama
shirikisho la mpira wa miguu Tanzania tumepata kiongozi Gianni Infantino
na tunaamini tutasonga mbele”.
Shaffihdauda.co.tz: Infatino
amekuwa rais wa FIFA, sera zake zinaiangalia Afrika na Tanzania kwa
ujumla au kwasababu amekuwa rais inabidi twende nae hivyohivyo?
Malinzi:
Rais wetu Gianni Infantino aliongea mambo mengi sana kwenye manifesto
kwa maana ya ilani. Ukisoma ilani yake imezungumzia mambo makubwa sana
siyo kwa ajili ya Afrika lakini kwa ajili ya mpira wa dunia lakini
kikubwa kuliko vyote ni kwamba, rais wetu Infantino sasa ni muda wake wa
kubadilisha mpira wa Afrika, Asia, Oceania, Amerika Kusini na Kati na
Ulaya na dunia kwa ujumla.
Ndiyo muda sasa wa kutuunganisha ili mpira uweze kuonekana ukichezwa kwa umoja kwa maana ya dunia.
Shaffihdauda.co.tz:
Kabla ya zoezi la kupiga kura kuanza, watu wengi walikuwa wanampa
nafasi Sheikh Salman hasa baada ya bara la Afrika kuonekana kum-support
ambalo ndiyo block lenye kura nyingi pamoja na bara lake la Asia, lakini
Sheikh Salman tangu mwanzo kabisa alipata kura chache dhidi ya
infatino. Nini kimetokea kwa mtazamo wako?
Malinzi: Shirikisho la
soka barani Afrika walitoa tamko kwa maana kamati ya utendaji ya CAF
kwamba wanam-support Sheikh Salman, lakini tamko ni tamko na wapiga kura
ni wapiga kura. Wapiga kura wameamua kufanya walichokifanya na niseme
tu kwamba uchaguzi umekwisha kilichobaki tucheze mpira.
Post a Comment