HABARI ZA HIVI PUNDE
Mhariri wa Mlimani TV, Hamis Dambaya amepoteza mke na mtoto katika ajali ya barabarani iliyohusisha basi la Simba Mtoto na lori. Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania-TEF, NEVILLE MEENA, imeeleza kuwa katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi, pia Mama Mkwe wa Damumbaya amefariki dunia.
AJALI TANGA: Watu 11 Wafa, 18 wajeruhiwa baada ya basi la Simba Mtoto toka Tanga kwenda Dar kugongana na lori huko Muheza, Kamanda Mihayo Msikhela athibitisha.
#Habari za hivi punde:Ajali mbaya imetokea kati ya Muheza na Hale Tanga asubuhi hii na inasadikiwa imeuwa na kujeruhi.
Ajali hiyo imehusisha Basi la Simba Video na Lori na inaelezwa kwamba
madereva wote pamoja na utingo wa magari yote mawili wamepoteza maisha.
#Updates
Ajali:Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga amedhibitisha kutokea kwa ajali
ya basi la Simba Mtoto na Watu kadhaa wamejuruhiwa katika ajili hiyo na
wengine kadhaa waahofiwa kupoteza maisha.
TAARIFA ZAIDI TUTAWALETEA:
CHANZO:Habari Star TV Tanzania
Post a Comment