Kulia ni mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Iringa Cyprian Kuyava akiwa na baadhi ya viongozi wa uwanja wa samora.
NA FREDY MGUNDA,IRINGA
Chama
cha mpira wa miguu mkoa wa Iringa (IRFA) kiko mbioni kujenga uwanja wake
wa kisasa utakaosaidia kuendeshea ligi mbalimbali zikiwemo ligi za
kimataifa hali itakayosaidia kuinua soka la mkoa huo .
Akizungumza
ofisini kwake mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Iringa
Cyprian Kuyava alisema wameamua kujenga uwanja wao ili kuepukana na adha
wanayopata kutokana na kukosa sehemu ya kuendeshea ligi mbalimbali .
Alisema
tayari wameshapata eneo la hekari 14 katika eneo la kitwiru ndani ya
manispaa ya Iringa na sasa kinachosubiriwa ni kumaliza mazungumzo kati
ya chama hicho na manispa ya Iringa ili kuweza kumilikishwa eneo hilo
ili liwe mali yao kabisa tofauti na apo awali ambao manispaa hiyo
ilikuwa inataka kuingia nao ubia.
“Tayari
hili swala liko katika hatua za mwisho na tayari tumesha fanya
mazungumzo tunataka tujenge uwanja wetu wenyewe wa kisasa ambao tunaweza
kucheza mechi za kimataifa kwani tumekuwa tukipata tabu ya viwanja vya
kuchezea na hii imechangia kwa kiasi kikubwa kuuwa soka la mkoa wetu
”alisema Kuyava
Alisema
wanasubiri majibu ya maombi waliyopeleka katika manispaa hiyo ili
kuweza kupunguziwa bei li kuanza mchakato wa kulipa fidia kwa wamiliki
wa maeneo hayo ili waanze mchakato wa uwanja huo wa kisasa .
Alisema
kuwa mara nyingi timu zimekuwa hazi pati kitu wanapotumia viwanja vya
watu kwani asilimia 16 za mapato yanayopatikana kutokana na kingilio
huchukuliwa na wamilika wa kiwanja na asilimia ndogo inabaki ndio
zinagawanywa katika maeno mengine na kujikuta timu hazinufaiki na
chochote .
Alisema
kuwa hapo awali walikuwa wakitumia uwanja wa samora ambao bado uko
katika matengenezo tena ya kusuasu kwa kuwa mpaka sasa bado wanadai
kusubiri nyasi za kupanda jambo litakalorudisha michezo nyuma endapo
hawatakuwa na maono ya kuwa na kiwanja chao wenyewe .
Kwa
upande wa wadau wa soka mkoa wa Iringa Ally salehe ambaye pia ni shabiki
wa timu ya lipuli anasema kuwa endapo juhudi za makusudi zitafanyika na
kufanikisha ujenzi wa uwanja huo basi ni dhahiri kuwa soka la mkoa wa
iringa litapanda kwa kiasi kikubwa .
Alisema
kuwa katika mkoa wa Iringa kuna vipaji vingi vya michezo ikiwemo
wachezaji wa mpira wa miguu lakini wamekuwa wakikosa sehemu za kufanyia
mazoezi ili kukuza vipaji vyao hivyo kujengwa kwa uwanja huo wa kisasa
utafungua fursa za ajira kwa vijana wengi.
Post a Comment