Bw.
Lawrence Mafuru Msajili wa Hazina akishuka kwenye gari wakati
alipowasili kwenye mradi wa Eco Residence ulioko Kinondoni Hananasifu
unaojengwa na shirika la Nyumba la Taifa NHC huku akiongozwa na
Mkurugenzi wa shirika hilo Bw. Nehemia Mchechu tayari kwa ukaguzi wa
jengo hilo ambalo nyumba zake zote zimeshauzwa na linatarajiwa
kukabidhiwa hivi karibuni kwa Shirika hilo.
Akizungumza
na Vyombo vya habari mara baada ya ukaguzi wa jeno hilo Msajiri wa
Hazina Bw. Lawrence Mafuru amepongeza uongozi wa NHC kwa kazi kubwa
wanayoifanya ambapo wamefanikiwa kujenga majengo yenye tahami ya
shilingi Trilioni 3.5 kutoka umiliki wa mwanzo ambapo kulikuwa na
majengo yenye thamani ya shilingi trilioni 1.
Mkopo
uliotumika kugharamia ujenzi wa majengo hayo mapya kutoka mabenki
mbalimbali ni jumla ya shilingi Bilioni 300 ambazo kiasi cha shilingi
Bilioni 100 zimeshalipwa tayari katika mabenki hayo na kiasi cha
shilingi bilioni 200 zinaendelea kulipwa
Naye
Mkurugenzi wa Shirika hilo Bw. Nehemia Mchechu amesema shirika hilo
linao mpango mkubwa wa ujenzi wa nyumba 500 za gharama nafuu kwa ajili
ya watanzania wenye kipato cha chini ambazo zitaanza kujengwa mwaka huu
huko Luguruni wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam..(PICHA NA JOHN
BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Bw.
Lawrence Mafuru Msajili wa Hazina akimsikiliza Violet Mafuwe Msanifu wa
majengo kutoka kampuni ya CPI Iternational ambaye pia ni Meneja Mradi
wa Eco Residence wakati alipokagua ujenzi wa jengo hilo.
Bw.
Lawrence Mafuru Msajili wa Hazina akimuuliza jambo Mkurugenzi wa NHC
Bw. Nehemia Mchechu mambo mbalimbali kuhusu miradi ya shirika
hilo wakati alipokagua ujenzi wa jengo hilo.
Bw.
Lawrence Mafuru Msajili wa Hazina akisikiliza maelezo ya Mkurugenzi wa
NHC Bw. Nehemia Mchechu wakati alipokagua ujenzi wa jengo hilo.
Bw. Lawrence Mafuru Msajili wa Hazina akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo hilo.
Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba NHC akifafanua jambo kwa waandishi wa habari mara baada ya Msajili wa Hazina kukagua mradi huo.
Bw.
Lawrence Mafuru Msajili wa Hazina akiagana na Mkurugenzi wa NHC Bw
Nehemia Mchechu mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo hilo.
Jengo linavyoonekana kwa nje.
Post a Comment