Waziri
wa ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mtaa,George
Simbachawane akizungumza na waandishi wa Habari
--
WAZIRI
wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mtaa,George
Simbachawane amewasimamisha kazi wakurugenzi wa nne ambao ni Elizabeth
Kitundu wa Halmashauri za Misenyi mkaoni Kagera,
Ally Kisengi wa Halmashauri ya Nanyumbu mkaoni Mtwara, Abdalla Mfaume wa Halmashauri ya Mbogwe mkoani Geita, baada ya kubainika wakurugenzi hao wametenda kosa la kuwahonga wakaguzi wa fedha kutoka katika ofisi ya Mkaguzi mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) ili wapewe hati safi huku Halmashauri hizi zikiwa na ufisadi .
Pia, Waziri Simbachawene amemsimamisha kazi mkurugenzi Halmashauri ya Tunduma Mkoani Mbeya Bi Halima Ajali ili kupisha uchunguzi kutokana matumizi mabaya ya madaraka.
Hata
hivyo Waziri Simbachawane pia ameziagiza mamlaka husika kuwasimisha
kazi watendaji wa ofisi ya mkaguzi wa Hesabu za Serikali nchini,CAG waliohusika kupokea rushwa kutoka kwa wakurugenzi hao ili watoe hati safi kwenye Halmashauri hizo huku zikiwa na ubadilifu wa fedha za Umma.
Akizungumza na waandishi wa habari mda huu Jijini Dar es Salaam,Waziri Simbachawene amesema Wakurugenzi hao wamegundulika baada ya uchunguzi wa kina uliofanywa na wizara yake,
Waziri Simbachawene ameyataja makosa yao kila mmoja wao ambapo amesema Mkurugenzi wa Halmashauri ya Misenyi, Bi Chitundu ametenda ametanda kosa baada ya kumwagiza mweka
hazina wake Majaliwa Bikwato atoe rushwa ya Milioni tatu kwa maafisa ya
(CAG) kwa lengo la kuficha kasoro walizoziabini katika ukaguzi huo ,
Ambapo Maafisa hao wa CAG waliopeka pesa hizo ni Stevin Buawa,John Elias pamoja na Kilembi Mkole,
Waziri Simbachawene amesema Katika Halmashauri ya Nanyumbu ambapo ameidai tarehe
26 Juni 2015 mkurugenzi wake bwana Kasengi pamoja na mweka hazina Pasco
Malowo na mwasibu Emmanuel Mugesa wamlimkabidhi fedha ya Milioni 3 na
laki tano afisa wa CAG ambapo afisa huyo alipokea pesa hizo kwaniaba
ya wenzake kwa lengo la kutoa hati safi,
Sanjari na huyo pia Waziri Simbachawene amesema hata katika Halmashauri ya Mbogwe mkoani Geita ambapo amedai mwezi
Novemba mwaka jana , Mkurugenzi wa Halmahsauri hiyo Abdalla Mfaume na
mweka hazina wake wamliwapat ia fedha maafisa wakaguzi wa C AG ambao
walipokea rushwa ya milioni 16 ili wafiche ufisadi walioubaini,
Hata
hivyo Simachawene amesema katika Halmashauri hiyo pia kumegundulika
kuwepo na ufisadi mkubwa ukiwemo malipo ya mishahara hewa pamoja na
malipo ya milioni 200 yaliotolewa pasipo kuwa na Stakabadhi ,
Aidha,Waziri Simbachawene amesema katika wilaya hiyo ambapo mkaguzi wa mkoa wa Geita alipewa Rushwa kutoka kwa viongozi wa wilaya hiyo ili kuficha ufisadi wa milioni 90 ambazo zilitengwa kwa ajili ya kununulia dawa.
Katika hatua nyingine Waziri Simbachawene amesema Kwa
mamlaka aliyekuwa nayo amemasiamisha kazi pia mkurugenzi wa Mji wa
Tunduma Bi Halima Ajali baada ya kubainika kutumia vibaya madaraka
aliyokuwa nayo.
Amesema
Mkurugenzi huyo alikuwa anawatumia watoto wake kwenye shughuli za
Halmashauri huku akiwalipa pesa pamoja na kuikosesha mapato Halmashauri
hiyo yaliyotokana na Ushuru wa Magari kwenye Mpaka wa Tunduma,
Vilevile waziri Simbachawene amemteua Erick
Mpunda kukaimu nafasi ya mkurugenzi huyo ambapo Mapunda kabla ya
kuteuliwa kwake hapo alikuwa Mkuu wa Rasilimali watu wmkoani Mbeya.
Waziri
Simbachawene amemuagiza Katibu kongozi kuwasimamisha watendaji wote
ambao walihusika na rushwa hizo kwenye ofisi ya CAG kwa madai kuwa wapo
kwenye Mamlaka yake,
Post a Comment