Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MKE WA RAIS WA VIETNAM ATEMBELEA OFISINI KWA MAMA MAGUFULI NA MAKUMBUSHO YA TAIFA

Mke wa Rais wa Vietnam, Mama Mai Thi Hahn akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Janeth Magufuli zilizopo Ikulu, Dar es Salaam. Mama Mai Thi Hahn ameambata na Mhe. Rais wa Vietnam Toung Tang San ambaye yupo nchini kwa ziara ya siku 4 kuanzia tarehe 8 Machi 2016.
Mama Mai Thi Hahn akiwasalimia wanawake waliokuja kumlaki katika ofisi za Mhe. Mama Magufuli.
Mama Mai Thi Hahn akisalimiana na mmoja wa wasanii wa vikundi vya ngoma vilivyofika kumlaki katika eneo la Ofisi za Mama Magufuli
Mama Mai Thi Hahn akieleza umuhimu wa ziara yake na Mhe. Rais Toung Tang San ambapo alisema lengo la ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano  wa kihistoria uliopo kati ya nchi yake na Tanzania.
Mama Magufuli akimkabidhi Mama Mai Thi Hahn zawadi ya Kinyago mashuhuri cha "Umoja" kilichochongwa nchini Tanzania.
Pia Mama Mai Thi Hahn naye alikabidhi zawadi kwa Mama Magufuli.
Wake za Marais wakicheza ngoma na kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitumbuiza ofisini hapo.
Mama Hahn na Mama Magufuli wakiagana na kina mama (hawapo pichani) mara baada ya kutembelea ofisini

 ..........Alipotembelea Makumbusho ya Taifa

Mama Hahn na Mama Magufuli wakisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Makumbusho ya Taifa mara baada ya kuwasili.
Mama Mai Thi Hahn akisaini kitabu cha Wageni katika Ofisi za Makumbusho za Taifa
Mwenyeji wake Mama Janeth Magufuli naye akisaini kitabu cha wageni katika ofisi hizo.
Wakipokea maelezo ya Michoro kutoka kwa afisa wa makumbusha ya Taifa hayupo pichani inayoeleza historia ya nchi ya Tanzania na namna Wasanii walivyoweza kuwa wabunifu kwa kuchora picha nzuri zinazoeleza historia ya Taifa.
Afisa wa Makumbusho akiendelea kuelezea michoro mingine na maana zake ambapo makumbusho hiyo imekuwa ikihifadhi kumbukumbu hizo kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo katika kurithisha historia na wageni kuweza kuijua historia ya Tanzania
Wakiendelea kupokea maelezo.
Wakielezewa na Afisa wa Makumbusho ya Taifa  kuhusu picha zinazoonyesha historia ya utumwa ambapo wakati wa Ukoloni Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi ambazo watumwa walichukuliwa.
Maelezo juu ya  biashara ya pembe za ndovu enzi za ukoloni  yakiendelea kutolewa.
Mara baada ya kumaliza ziara hiyo Wake za Marais kwa pamoja walikabidhiwa zawadi ya vikapu vya asili na ofisi ya Makumbusho ya Taifa.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top