Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Taarifa ya Ofisi ya Spika kuthibitisha kupokea hoja ya kumeondoa madarakani Naibu Spika

Ofisi ya Spika imepokea taarifa ya kusudio la kuleta Bungeni Hoja ya kumwondoa madarakani Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) iliyowasilishwa na Mbunge wa Simanjiro Mhe. Mhe. James Kinyasi Millya siku ya Jumatano tarehe 1 Juni, 2016.

Utaratibu huo ni wa Kikatiba na upo chini ya Ibara ya 85(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 ambapo pia umeainishwa katika Kanuni ya 138 (1), ya kanuni za Kudumu za Bunge kuhusu utaratibu wa Kumwondoa Naibu Spika Madarakani.

Baada ya kupokea kusudio hilo, Kanuni za Bunge zinamtaka Spika kuiwasilisha hoja hiyo katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili ifanyiwe kazi.

Kutokana na msingi huo wa kikanuni, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (Mb) anakusudia kuliwasilisha swala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kama Kanuni inavyoelekeza ambapo kamati hiyo itaangalia msingi wa hoja na endapo itaridhika, kanuni inaitaka Kamati kuwasilisha hoja hiyo Bungeni ili ijadiliwe.

Aidha, Kanuni ya 138 (3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, inamtaka Spika kukalia kiti wakati wa mjadala wa hoja ya kumwondoa Naibu Spika Madarakani.

Hivyo basi, suala lililowasilishwa na Mhe. James Kinyasi Millya kuhusu kusudio la kumwondoa Naibu Spika Madarakani, tayari limepokelewa na lipo katika Ofisi ya Spika kwa ajili ya utekelezaji wa masharti ya Kanuni.

Imetolewa na,
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
Ofisi ya Bunge
DODOMA
6 Juni, 2016.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top