Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TAARIFA YA SERIKALI KUHUSIANA NA TUHUMA ZA VYOMBO VYA HABARI KUWA MELI ZA IRAN ZINAPEPERUSHA BENDERA TANZANIA


Serikali imepokea taarifa kuhusu tuhuma za meli za Iran kupeperusha bendera za Tanzania ili kukwepa vikwazo

Serikali ya Jamhuri ya Muungano na SMZ hazitaki kupuuza taarifa hizi. Serikali zote mbili zimeamua kufanya uchunguzi ili kuthibitisha

Tanzania imewaarifu nchi zilizolalamika marafiki kuwaomba kusaidiana nasi kufanya uchunguzi na kushirikiana kuthibitisha taarifa hii

Tumefanya hivyo kwa kuzingatia uwezo wetu wa kiutafiti na kutaka utafiti huu kuwa huru kwa kuwashirikisha wao wenye ujuzi mkubwa

Tunafanya hivyo kwa kuwa wakala wa ZMA anayefanya kazi za kusajili amekana kusajili meli za Iran, Balozi wa Iran nchini aliitwa akakanusha

Tutakapopata matokeo ya utafiti na ikithibitika kuwepo na ukweli hatua zitachukuliwa mara moja

Tukithibitisha tuhuma hizi tutafutilia mbali usajili wa meli hizo

Hatufanyi haya kutokana na barua ya congressman, tunafanya hivyo kutimiza wajibu wetu kimataifa hususan Azimio 1920 la UN Security Council

Tanzani sio adui wa nchi yoyote duniani. Tunafurahia mahusiano yetu na nchi zote duniani

Hili ni jambo linalogusa maslahi ya Tanzania nje na maslahi ya Tanzania ya ndani (Muungano), tujihadhari na namna tunavyolizungumzia

Tusimame pamoja kama taifa. Nchi kwanza!
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top