Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

LEMA AZIDI FUNGUA MATAWI HUKO ARUSHA,HUKU AKIPINGA KUVULIWA UBUNGE WAKE KWA HOJA 42

Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini kabla ya Mahakama kutengua Ubunge wake, Mh Godbless Lema amefungua matawi katika Kata ya Daraja Mbili Jijini Arusha juzi August 18,2012.
Katika ziara hiyo, Lema aliambatana na Mbunge wa Arumeru Masariki Mh Joshua Nassari pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM kabla ya kujiengua na kujiunga na Chadema mapema mwezi Aprili mwaka huu, Ndg James Ole Millya, ambao nao kwa nyakati tofauti walipata fursa ya kuzunumza.
Mbali na suala la uzinduzi na upokeaji wanachama wapya, Lema alifanya harambee ya kukusanya fedha kusaidia shughuli za chama hicho katika Kata hiyo ambapo jumla ya Sh 219,500 zilichangwa na wananchi.
Akiondoka eneo hilo, Lema alilazimika kuwatuliza mamia ya watu waliokuwa wanafuatilia msafara wake ili kuepusha kutokea mwanya kwa watu wenye nia mbaya kuleta vurugu na uharibifu wa mali. Baadae msafara wake  ulikatiza mitaa ya Stand Kuu ya mabasi makubwa na kisha kuelekea bustani ya City Park huku njiani akishangiliwa sana na baadhi ya watu wakinyoosha vidole  kama ishara ya ushindi.
Huku akiendelea na mikutano hiyo Lema amewasilisha hoja 42 kupinga kuvuliwa Ubunge wake wa Arusha Mjini katika shauri litakalo somwa septemba 20 Mwaka huu.
Lema alivuliwa Ubunge na MAKAHAMA Kuu Kanda ya Arusha,  iliyotengua matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi mgombea wa Chadema, Godbless Lema baada ya kuridhika kuwa alitumia lugha ya kashfa na udhalilishaji dhidi ya aliyekuwa mpinzani wake katika uchaguzi huo wa mwaka 2010, Dk Batilda Burian.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top