Mbunge wa Monduli Mh.Edward Lowassa akiongea wakati wa Harambee ya Kuchangia Ujenzi wa Kanisa la KKT usharika wa Babati,Mkoa wa Manyara jana.
(Picha na Michuzi Blg)
Ni kuhusu elimu bure hadi sekondari, asema iwe moja ya ajenda za ccm 2015
Kwa ufupi
Lowassa akizungumza jana mjini Babati alisema, 
mjadala kuhusu elimu kutolewa bure hadi sekondari haukwepeki, hivyo 
kuwataka wadau wa elimu kuanza sasa kujadili suala hilo na kwamba Chama 
Cha Mapinduzi (CCM) kinapaswa kulifanya hilo kuwa moja ya ajenda zake 
katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Lowassa akizungumza jana mjini Babati alisema, 
mjadala kuhusu elimu kutolewa bure hadi sekondari haukwepeki, hivyo 
kuwataka wadau wa elimu kuanza sasa kujadili suala hilo na kwamba Chama 
Cha Mapinduzi (CCM) kinapaswa kulifanya hilo kuwa moja ya ajenda zake 
katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Alisema elimu ya sekondari ikifanywa bure, itakuwa
 ni fursa kwa kila mtoto wa Kitanzania kuipata. Hatua ambayo itaongeza 
weledi na uelewa wa mambo mengi katika jamii.
“Ninasema sasa wakati umefika elimu ya sekondari 
kuwa kama elimu ya msingi kwa watoto kusoma bure kuanzia kidato cha 
kwanza hadi kidato cha nne,” alisisitiza Lowassa ambaye ni Mbunge wa 
Monduli (CCM).
Kwa kauli hiyo, Lowassa ni kama ameunga mkono Sera
 ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao waliingia katika 
mgogoro na CCM kuhusu elimu kutolewa bure wakati wa kampeni za Uchaguzi 
Mkuu wa 2010.
Chadema wamekuwa wakisisitiza kwamba elimu bure 
inawezekana hadi ngazi ya sekondari, lakini wakati wote CCM wamekuwa 
wakisema kuwa suala hilo haliwezekani na kwamba kauli za aina hiyo ni 
kuwahadaa wananchi.
Katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, aliyekuwa mgombea wa
 urais kupitia Chadema, Dk Willibrod Slaa alitumia sera ya elimu bure 
kuanzia chekechea hadi sekondari kama kete ya kusaka ushindi, huku 
akisema chama chake kingetenga asilimia 35 ya bajeti kwa ajili ya 
kuboresha elimu na kutoa elimu bure.
Hata hivyo, aliyekuwa mgombea wa CCM na baadaye 
kupata ushindi, Rais Rais Jakaya Kikwete alikuwa akiwatahadharisha 
wapigakura kuwa kwamba ahadi ya Chadema ni hewa na kwamba hilo 
lisingewezekana.
Mvutano huo uliwaingiza makada wengine ambao ni 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ambaye wakati huo alikuwa Meneja 
Kampeni wa CCM na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel 
Sitta na kwa upande wa Chadema, Dk Kitila Mkumbo naye alijitokeza 
kutetea sera ya chama chake.
Katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika 
Novemba 10, 2010 katika Kata ya Mchangimbore katika Jimbo la Peramiho 
mkoani Ruvuma, Rais Kikwete alisema “Serikali haiwezi kutoa huduma za 
jamii bure” na kwamba lazima wananchi wachangie.
“Nimebahatika kukaa serikalini muda mrefu hiyo 
sera ya bure tulijaribu na ikatushinda na wakati huo Hayati Baba wa 
Taifa, Mwalimu Nyerere, tulikaa naye tukaona hilo haliwezekani tukaamua 
tubadilishe sasa nawashangaa wenzetu wanawadanganya eti watatoa bure.”
Kwa upande wake Dk Slaa akiwa mjini Arusha katika 
moja ya mikutano yake alisema kwamba CCM walikuwa wakipinga sera ya 
elimu bure hadi sekondari kutokana na kulea ubadhirifu na kuthamini 
anasa kuliko maendeleo kwa wananchi.
Kauli ya Lowassa
Jana akizungumza muda mfupi kabla ya kuanza kuendesha harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Babati, Lowassa alisema wakati umefika kwa kila Mtanzania kuzungumzia suala hilo bila ya woga.
Kauli ya Lowassa
Jana akizungumza muda mfupi kabla ya kuanza kuendesha harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Babati, Lowassa alisema wakati umefika kwa kila Mtanzania kuzungumzia suala hilo bila ya woga.
"'Ni lazima tukubali na tujadili suala hilo kwa manufaa ya nchi 
kwa kila Mtanzania kukubali ushauri huo wa elimu ya sekondari kuwa ya 
bure,” alisema Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli (CCM) na 
kuongeza:
“Tukishakuwa na mjadala wa elimu yetu kuwa bure 
hadi ngazi ya sekondari, tena basi iwe ni elimu bora, jambo hili 
linapaswa kuwa moja ya ajenda kuu za CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.”
Alisema Serikali inapaswa kugharimia elimu ya 
sekondari bila ya woga na kwamba anaunga mkono wito uliotolewa hivi 
karibuni na Rais Jakaya Kikwete akiwaagiza watendaji serikalini 
kusimamia ujenzi wa maabara katika shule za sekondari za kata.
Alisema mafanikio katika ujenzi wa shule za kata 
nchini yanatokana na mpango ambao yeye ni mwasisi wake alipokuwa Waziri 
Mkuu na kwamba ali aliusimamia kikamilifu kuhakikisha unafanikiwa.
Azungumzia tuhuma
Katika hatua nyingine, Lowassa alizungumzia tuhuma zinazoelekezwa kwake kwamba ana utajiri wa kupindukia kwamba siyo za kweli na zinalenga kumpaka matope.
Azungumzia tuhuma
Katika hatua nyingine, Lowassa alizungumzia tuhuma zinazoelekezwa kwake kwamba ana utajiri wa kupindukia kwamba siyo za kweli na zinalenga kumpaka matope.
Alisema wale wanaomtuhumu kutokana na yeye 
kushiriki katika uchangiaji wa shughuli za kijamii hawamtendei haki 
kwani kuchangia siyo kosa.
Lowassa alisema anachokifanya yeye katika shughuli
 anayoalikwa huwataarifu marafiki zake kote nchini na kwenda katika eneo
 husika na kuchangia na yeye hana utajiri huo kama inavyodaiwa.
Alisema, ataendelea kuchangia bila ya wasiwasi 
yeye na marafiki zake na hatishwi na tuhuma hizo kwani siyo za kweli na 
aliziita kuwa ni  ‘uongo wa kupindukia’.
Naye Askofu wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini 
Mashariki, Dk Thomas Laizer aliwataka waumini wa kanisa hilo kote nchini
 na waumini wa makanisa mengine kuwapuuza baadhi ya watu wenye kutaka 
kuleta vurugu nchini.
Askofu Laizer alisema vurugu za kuchoma makanisa 
zilizofanyika Mbagala na maeneo mengi zinapaswa zikomeshwe, lakini 
akatoa wito kwa waumini Waksrito walioguswa kutokuwa na mawazo ya 
ulipizaji wa kisasi.
Alisema, nchini kuna Waislamu wengi wasiounga 
mkono vitendo vinavyodaiwa kufanywa na baadhi ya waumini wa dini hiyo, 
hivyo makanisa yaombee amani ya nchi, ili Watanzania waendelee kuishi 
kwa utulivu.
“Kila mtu mwenye dini afanye maombi kuiombea nchi 
amani, yapo makanisa mengi yamechomwa moto na siyo kama waumini wa dini 
ya Kikristo ni waoga la hasha, bali mafundisho yetu yanakataza ulipizaji
 wa kisasi, kisasi ni kwa ajili ya Mungu,” alisema Askofu Laizer.
Katika harambee hiyo kiasi cha Sh133. 89 milioni 
kilichangwa, na kati ya hizo Sh87. 54 ni fedha taslimu na Sh45.85 ni 
ahadi. Fedha hizo ni zaidi ya malengo yaliyokuwa yamekusudiwa ya 
kuchangisha Sh120 milioni.
Hadi sasa ujenzi wa kanisa hilo umeshagharimu Sh186 milioni na hadi litakapokamilika linatarijiwa kuwa limegharimu kiasi cha Sh600 milioni.
Hadi sasa ujenzi wa kanisa hilo umeshagharimu Sh186 milioni na hadi litakapokamilika linatarijiwa kuwa limegharimu kiasi cha Sh600 milioni.
Chanzo:Mwananchi.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment