Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CHADEMA YAZIDI KUJIIMARISHA ARUSHA

DSCN6510Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Ndg Amani Golugwa akipeana mkono na Mwenyekiti wa Kamati iliyoratibu hafla ya kuwakutanisha marafiki wa Chadema Arusha na nje ya Mkoa huo katika Hoteli ya Kitalii ya Snow Crest ya Jijini Arusha jana, kama ishara ya kushukuru kupokea vifaa mbalimbali vya muziki na matangazo ambavyo vitatumika kwa shughuli za chama katika kueneza vuguvugu la mabadiliko (M4C) kama linavyohubiriwa na chama hicho.

Kwa maelezo ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mh Godbless Lema, vifaa hivyo ni seti kamili pamoja na jenerator kubwa vinathamani ya zaidi ya Shilingi za Kitanzania Milioni 14, pesa ambazo zilitoka kwa marafiki hao na baadhi ya viongozi wa chama.


Akishukuru kupatikana kwa vifaa hivyo, Golugwa aliwasifu marafiki hao kwa moyo wa kujitolea kwa lengo la kusaidia nchi yao, na yeye kuahidi kutoa Sh milioni moja kusaidia upatikanaji wa gari aina ya FUSO kwa ajili ya kubebea vifaa hivyo.


Chadema Arusha kupitia Kamati maalulu waliangaa mjumuiko huo wa marafiki na kuupa jina la “M4C Join The Chain” ukimaanisha kuwataka wananchi wote wanaokerwa na hali halisi ya mambo ilivyo wajiunge na harakati za Chadema kisiasa ama kwa kushiriki kugombea nafasi za uongozi au kusaidia harakati hizo kwa namna watakavyoweza.


Mjumuiko huo uliwakutanisha marafiki mbalimbali wa ndani ya Arusha na nje ya Mkoa wakiwemo baadhi ya wafanya biashara wakubwa Jijini hapa. Chadema Makao makuu waliwakilishwa na Mwenyekiti wa Chadema Kanda Maalumu ya dar es Salaam, Henry Kileo, huku viongozi wengi wa Chadema Arusha na madiwani wote wakihudhuria, smbamba na Mh Lema na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari.


Awali kulikuwa na hotuba za kutia hamasa kutoka kwa wazungumzaji mbalimbali walioandaliwa, aliwemo dada yake na Hussein Bashe, Kauthar Mohamed Bashe aliyewapa ujasiri wanawake kushiriki nafasi za uongozi kisiasa na kuwa sehemu ya maamuzi katika jamii bila kuwaachia wanaume pekee.


Wazungumzaji wengine walikuwa ni pamoja na mwanadada aliyejitambulisha kama Aminata kutoka Korogwe Tanga ambako ana nia ya kuwania Jimbo la Korogwe katika uchaguzi mkuu ujao, pamoja na Emma Mroso aliyezungumzia tatizo la hofu miongoni mwa watanzania.
DSCN6454Amani alisema Chadema kwa sasa inahitaji kwenda kwa watu na kuwaonesha kuwa wana dhamira ya dhati ya kupigania maslahi ya Tanzania na watu wake na kuahidi kuwa watathakikisha wanasimamia Halmashauri zote wanazoziongoza ili ziwe za mfano kwa vyama vingine kwa misingi ya ufanisi katika kutumikia jamii.


Katika hitimisho lake Katibu huyo alitoa taarifa ya kusudio la chama chake kuwa na Wiki ya Chadema itakayofikia kilele siku ya Januari 23, 2013 siku ambayo Chadema itatimiza miaka 20 tangu kupatiwa usajili wa kudumu kama chama cha siasa nchini.
DSCN6468Mh Godbless Lema, mjumbe wa Kamati Kuu Chadema akifafanua jambo katika hafla hiyo. Pamoja na mambo mengine, Lema alijikita zaidi kuelezea namna harakati za chama chake zinavyokutana na vikwazo vingi kiasi cha kulazimisha kufikiria namna ya kujitegemea.

Akizungumzia upatikanani wa vifaa hivyo binafsi, Lema alisema kukodisha vifaa ni gaharama kubwa sana kiasi cha sh laki nne kwa kila mkutano na kudai kuwa chama hakina uwezo huo na hivyo njia mbadla na nafuu ni kuwa na vifaa vyao wenyewe. yeye na marafiki zake binafsi aliodai atawatafuta aliahidi kuchangia milioni 5 katika uchangishaji mwingine kwa ajili ya kupata gari la matangazo yao ambalo watalitumia kuzunguka maeneo tofauti ya nchi.


Lema laikumbushia vikwamishi walivyowahi kukutana navyo katika utaratibu wa awali wa wananchi kuchagia chama chake kwa kutumia namba 15710 ambapo alieleza kuwako kwa shinikizo toka Serikalini kwa makampuni ya simu kuwa katika makusanyo yote Chadema wapewe aslimilia 20 tu.

Chanzo:Noise of Silence Blog
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top