Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CHADEMA:HATUKUFANYA YA MAGUFULI

 Waziri Mkuu wa Kenya na mgombea urais wa Muungano wa CORD, Raila Odinga akimkaribisha Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kushoto) kwenye mkutano wa CORD uliofanyika juzi katika Viwanja vya Uhuru, jijini Nairobi.
 Na Mpiga Picha Wetu Hisani kubwa ya Mwananchi
,,,,,,,,,,,
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, alihudhuria mkutano wa kampeni wa Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) nchini Kenya kama chama rafiki kwa mwaliko wa Raila Odinga.
CHADEMA ilifafanua kuwa Mbowe aliteuliwa na Kamati Kuu na wala hakutoa kauli yoyote kwenye mkutano huo ya kuwashawishi Wakenya wamchague Odinga kama alivyofanya Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, alipohudhuria mkutano wa chama hicho Decemba 7 mwaka huu.
Magufuli akiwa amealikwa kibinafsi kama rafiki wa Odinga alitoa kauli ya kumpigia debe kiongozi huyo akitaka Wakenya wamchague na kwamba Watanzania wanamuunga mkono.
Hata hivyo kauli hiyo iliibua mtafaruku huku baadhi ya watu wakiwemo CHADEMA wakihoji kama ilikuwa ya serikali na kumtaka Rais Jakaya Kikwete atolee ufafanuzi, vinginevyo nchi ingekuwa na uhusiano mbaya na Kenya, endapo Raila hatachaguliwa kuwa Rais.
Akizungumza na Tanzania Daima, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Habari wa CHADEMA, John Mnyika, alisisitiza kuwa Mbowe alihudhuria kampeni za ODM kwa niaba yao na kwamba alipewa baraka zote na Kamati Kuu.
Alisema hatua hiyo ni tofauti na ile ya Magufuli ambaye alialikwa kibinafsi na Odinga halafu akatoa kauli tatanishi za kuhatarisha uhusiano wa kidiplomasia bila kufafanua kama ni msimamo wake au serikali.
“Kwetu ODM ni chama rafiki kama ilivyo kwa vyama kadhaa barani Afrika na Ulaya. Mfano kwa Afrika vipo Democratic Turnhalle Aliance (DTA) cha Namibia, RENAMO cha Msumbiji, New Patriotic Party cha Ghana na Forum for Democratic Change cha Uganda.
“Kwa Ulaya vipo CDU kinachotawala nchini Ujerumani, KMT kinachotawala China, DP kinachotawala Albania, Republican chama cha upinzani nchini Marekani, Conservative cha Uingereza na Peoples Party cha Hispania,” alisema.
Mnyika aliongeza kuwa hoja yao haikuwa Waziri Magufuli kuhudhuria mkutano wa ODM ila kauli aliyoitoa ilikuwa ya kuweka shakani uhusiano wa Kenya na Tanzania endapo kitashinda chama tofauti na ODM.
Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo, aliongeza kuwa ndiyo maana CHADEMA kupitia kwa Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje, Ezekiel Wenje, iliitaka serikali ifafanue kama ilimtuma-katumwa na chama chake cha CCM au binafsi.
“Wenje alihoji kitendo cha Magufuli kupanda jukwaani kuanza kumnadi kiongozi wa ODM kuwa ni ukiukwaji wa kanuni na taratibu za kimataifa ambapo kwa mujibu wa kanuni hizo ni kosa kubwa taifa moja kuingilia siasa za taifa jingine hata kama hayo mataifa yana ushirikiano,” alisema.
Barua ya mwaliko wa Magufuli kutoka ODM ambayo Tanzania Daima imeiona inaonyesha kuwa alialikwa kibinafsi, hivyo hakukuwa na sababu kuwasemea Watanzania kama vile amebeba dhamana ya uwaziri katika mkutano ule.

NA TANZANIA DAIMA
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top