NAIBU Katibu
Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Lawrence Tara, amejivua uanachama wa
chama hicho na kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Tara ambaye
pia ni Diwani wa Kata ya Bashnet, wilayani Babati, Mkoa wa Manyara
tangu mwaka 2000, alitangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari
jana, baada ya kupokewa Chadema na Mjumbe wa Kamati Kuu wa chama hicho,
Godbless Lema.
Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na kiongozi mwingine wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini, Ally Bananga.
Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na kiongozi mwingine wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini, Ally Bananga.
Tara alitoa
sababu mbili zilizomfanya aihame NCCR-Mageuzi na kujiunga na Chadema;
upendeleo na dhuluma kwa watumishi wa chama hicho.
Alidai kwamba baadhi ya viongozi wa NCCR-Mageuzi wanaonyesha upendeleo wa wazi kwa kigezo cha urafiki kama kifanyavyo chama tawala, CCM.
Alidai kwamba baadhi ya viongozi wa NCCR-Mageuzi wanaonyesha upendeleo wa wazi kwa kigezo cha urafiki kama kifanyavyo chama tawala, CCM.
Alisema yeye
ni mmoja wa waathirika wa mfumo huo mbovu ndani ya NCCR- Mageuzi, baada
ya chama hicho kumtelekeza katika kudai haki yake ya ubunge aliyodai
kwamba iliporwa na CCM.
“Tunahitaji
chama cha siasa kilicho makini na ambacho Watanzania tunapaswa
kuunganisha nguvu zetu kwa pamoja bila kutengana na kwa maoni yangu
NCCR-Mageuzi siyo chama cha aina hiyo,” alisema Tara.
Akifafanua madai ya kudhulumiwa na CCM, Tara alidai kwamba alishinda ubunge wa Jimbo la Babati Vijijini, lakini akadhulumiwa.
Alisema katika mazingira hayo amebakiwa na chaguo mojawapo kati ya kubaki ndani ya chama kisichokerwa na hali hiyo na ambacho baadhi ya viongozi wake wanaendeleza upendeleo wa urafiki na undugu.
Alisema katika mazingira hayo amebakiwa na chaguo mojawapo kati ya kubaki ndani ya chama kisichokerwa na hali hiyo na ambacho baadhi ya viongozi wake wanaendeleza upendeleo wa urafiki na undugu.
“Nikaona
bora kujitenga na kuachana na chama chenye viongozi wa aina hiyo na
kutafuta chama imara ambacho hakina simile na mambo kama hayo. Pia
chenye kupigania haki, ukweli na ambacho kimepania utawala bora na
ustawi wa Watanzania,” alisema.
“Ninaamini Chadema ni chama makini kilichopania kutokomeza dhuluma, uovu na ufisadi wa kidola na kuleta ustawi wa Tanzania,” alisema na kuwaomba wakazi wa Bashnet, Manyara na
“Ninaamini Chadema ni chama makini kilichopania kutokomeza dhuluma, uovu na ufisadi wa kidola na kuleta ustawi wa Tanzania,” alisema na kuwaomba wakazi wa Bashnet, Manyara na
Watanzania kumuunga mkono.
Akizungumza katika mkutano huo, Lema alimpongeza Tara na kusema chama hicho sasa kimeongezewa nguvu.
Akizungumza katika mkutano huo, Lema alimpongeza Tara na kusema chama hicho sasa kimeongezewa nguvu.
“Huyu ni
sawa na Leonel Messi (mchezaji soka mahiri wa klabu ya Barcelona na
Argentina). Sasa huwezi kumleta achezee AFC ya Arusha na Babati Stars
halafu mpate mafanikio kutokana na mfumo uliopo, huyu anatakiwa awe
Manchester United au timu nyingine kubwa,” alisema Lema.
Alisema
viongozi wa chama chake badala ya kumpa ushirikiano ili aweze kushinda
ubunge, Mwenyekiti wake alikubali kupewa ubunge wa kuteuliwa na Rais na
hivyo Tara kuachwa mwenyewe.
“Uso
umeumbwa na haya kuna vitu ukishakula huwezi kupinga. Hivyo jambo bora
ni kuondoka huko na kwa hili nampongeza Tara kwa kuacha vyeo vyote
ikiwemo posho za vikao vya udiwani na posho ya kila mwezi,” alisema
Lema.
Alisema Tara
anatarajiwa kupewa kadi ya chama hicho na Mwenyekiti wa Chadema,
Freeman Mbowe au Katibu Mkuu wake, Dk Wilbroad Slaa kwa kuwa yeye hawezi
kufanya hivyo kutokana na nafasi kubwa aliyokuwa nayo mwanachama huyo
mpya.
Chanzo:CHADEMA BLOG
Post a Comment