Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

SAFARI ZA NDANI ZA NDEGE ZAREJEA KATIKA MAENEO YALIYOKOMBOLEWA KUTOKA KWA AL-SHABAAB

Na Majid Ahmed, Mogadishu

African Airlines, shirika la ndege linalomilikiwa na wafanyabiashara wa Somalia, limeanza safari za ndani katika maeneo yaliyokombolewa kutoka kwa al-Shabaab, likiwa ni la kwanza kwa kampuni kama hizo kutumia fursa baada ya kuimarika kwa hali ya usalama.

Ndege ya Turkish Airlines ikiwa imekaa kwenye barabara huko Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden Ade mjini Mogadishu. Kampuni ya ndani Afrikan Airlines imeanza safari za ndege katika maeneo yaliyokombolewa kutoka kwa al-Shabaab. [Na Mohamed Abdiwahab/AFP]

"Safari za ndani za African Airlines zitawaruhusu watu kufikia maeneo ambayo yalikuwa shida kuyafikia kupitia ardhini kutokana na ukosefu wa usalama, barabara mbovu au masafa marefu," alisema Mohamed Jama wa bodi ya wakurugenzi ya African Airlines.

"Shirika lilianza safari hizi za ndani hapo tarehe 4 Disemba baada ya kupata vibali zinazotakikana na kukubaliwa na serikali ya Somalia pamoja na Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia, ambao ndio wenye dhamana ya usalama wa viwanja vya ndege katika miji iliyokombolewa" aliiambia Sabahi.

Jama alisema kuwa kampuni ya African Airlines, ambayo mwanzo ilifanya safari kwenda Somaliland na Puntland tu, sasa inazo safari tatu za ndani kwa wiki kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden Ade kuelkea miji iliyokombolewa hivi karibuni ya Kismayu, Baidoa na Beledweyne. "Karibuni, kutakuwa na ratiba ya safari kwenda miji mingine yote ya Somalia ambayo ina viwanja vya ndege ambako ndege zinaweza kutua," alisema.

Mohamud Ahmed wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Somalia alisema kuwa safari hizo mpya zinaashiria kuwa hali ya usalama nchini inaimarika.

"Hali ya usalama nchini imeimarika sana tangu vikosi vya washirika kuichukua miji ya kimkakati ambayo ilikuwa katika udhibiti wa wanamgambo wa al-Shabaab," aliiambia Sabahi. "Biashara imeinuka karibu nchini kote na idadi ya Wasomali wanaorejea kutoka nje ili kuanzisha miradi ya uwekezaji imeongezeka kwa sababu ya kurejea kwa utulivu katika sehemu nyingi za nchi."


Kuinuka kwa uchumi wa ndani
Abdinur Osman, profesa wa uchumi katika Chuo Kikuu cha Green Hope mjini Mogadishu, pia alisema kuwa kuanza upya kwa safari za ndani kwenda maeneo yaliyokombolewa kati na kusini ya Somalia kumeinua uchumi wa ndani.

"Safari hizi mpya za ndani zinachangia kuimarisha biashara na ukuaji wa uchumi, pia kunaivutia wawekezaji wa Somalia na wa kigeni kushindana," aliiambia Sabahi.

Osman alitoa wito kwa serikali kuendeleza miundombinu ya viwanja vya ndege vikongwe katika miji iliyokombolewa hivi karibuni, ambapo isipokuwa uwanja wa ndege wa Mogadishu, viwanja vimechoka ma havijafanyiwa ukarabati tangu kuanguka kwa serikali kuu," alisema. "Kwa sababu hii, havikidhi viwango vya usalama vya kimataifa."

"Viwanja vya ndege ni njia [kuelekea duniani] na viwanja vikongwe vya ndege vinahitaji sana kukarabatiwa na kuimarishwa ili kuhamasisha safari nyingi zaidi na kuinua shughuli za biashara miongoni mwa mikoa kadhaa ya Somalia," alisema. "Kuimarisha idadi ya safari za ndani ili kuenea sehemu zote za Somalia kutasaidia kuunganisha miji ya Somalia na kuwahamasisha wawekezaji kuja kuwekeza nchini."

Mfanyabiashara wa Mogadishu Abdifatah Abdullahi alikaribisha uimarikaji huo baada ya kushindwa mfululizo kwa al-Shabaab.

"Wakati wa utawala wa al-Shabaab kwa mikoa ya kusini, ilikuwa ni vigumu kwa wafanyabiashara, maafisa wa serikali na viongozi wa kanda kufika katika maeneo ambayo yako mbali na mji mkuu, Mogadishu, au kutembea baina ya mikoa," aliiambia Sabahi. "Safari kwa kutumia barabara kutoka Mogadishu hadi Beledweyne ilichukua kiasi cha siku mbili, wakati kusafiri baina ya Mogadishu na Kismayu kunaweza kuchukua siku tatu hadi nne kutokana na barabara mbaya na masafa marefu."

"Sasa, kila mtu ataweza kufikia kirahisi maeneo yote," alisema. "Pia inapunguza muda unaotumiwa na wasafiri, kwa vile sasa wananchi wanaweza kufungua kinywa wakiwa Mogadishu na kula chakula cha mchana huko Kismayu, Beledweyne au Baidoa."

Abdullahi alisema kuwa waendesha biashara wa ndani kama vila Daallo Airlines, Jubba Airways na African Express Airways walikuwa wakifanya safari za ndani kwenda na kurudi kati na kusini ya Somalia, lakini safari zilikatishwa kutokana na kudorora kwa hali ya usalama wakati al-Shabaab ilipoichukua kusini ya Somalia miaka minne iliyopita.

Chanzo: sabahionline.com
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top