Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KILIMANJARO STARS YATANGULIA NUSU FAINALI YAIZABA RWANDA


Wafungaji wa mabao ya Stars leo, Kiemba kulia na Bocco kushoto wakipongezana baada ya kutupia kwenye nyavu.
Picha na Bongo Staz Blog
Mshambuliaji wa timu ya Kilimanjaro Stars inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Mrisho Ngasa aliyelala chini na wachezaji wenzake wakishangilia kwa staili ya aina yake baada ya kuwafunga Rwanda 2-0 katika mchezo wa Robo Fainali ya kwanza ya michuano ya Cecafa Challenge uliochezwa katika Uwanja wa KCC uliopo Lugogo nchini Uganda.
Picha na Shaffih dauda Blog.
 
FT: Kilimanjaro Stars 2-0 Rwanda. Shughuli imemalizika, Stars inatinga nusu fainali ya CECAFA.

 Watanzania waliopo uwanjani wanaimba "Tanzania Nakupenda Kwa Moyo Wote". Uzalendo kwanza.Hii ni kuonyesha kuwa njia ya Nusu Fainali iko nyeupe kuelekea Fainali
 
DK 90 + 2 Rwanda wanapata kona 
Dakika 90 zimemalizika zimeongezwa dakika 4 


DK 89' Kiemba anafanyiwa madhambi

Rwanda wanafunga bao linakataliwa

DK 86' Anaingia Shabani Nditi kuchukua nafasi ya John Bocco

Dak 85: Kilimanjaro Stars 2-0 Rwanda

Dk 82; TANZANIA 2 RWANDA 0
 
Kiungo mshambuliaji wa timu ya Kilimanjaro Stars inayadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Amri Kiemba na beki wa timu ya Rwanda, Michel Rusheshangoga wakiwania mpira wakati wa mchezo wa Robo  Fainali ya kwanza uliochezwa katika Uwanja wa KCC uliopo Lugogo nchini Uganda.
Picha na Shaffih Dauda Blog
 
DK 76' Rwanda wanapata free kick 

Stars wanaonekana kupoteza umakini na kuwaruhusu Rwanda kushambulia langoni

Dk 70: Kilimanjaro Stars 2-0 Rwanda

DK 66' John Bocco anapiga shuti kali golikipa wa Ndoli wa Rwanda anaokoa

DK 64 KILI STARS 2-0 RWANDA 

Kipindi cha pili sasa John Bocco anawapa raha  watanzania Kili Stars 2 Rwanda 0 

Dk 54: Goal Kilimanjaro Stars 2-0 Rwanda, John Bocco anasema nao Wanyarwanda kama kawaida nyota yake yazidi Kung'ara Bocco.

Salum Abubakar anatoka nafasi yake inachukuliwa na Athuman Idd Chuji ambae alikuwa anasubiriwa kwa hamu kubwa na mahsabiki nchini Uganda,

 Dakika 45 za kipindi cha pili zimeanza Kilimanjaro Stars 1-0 Rwanda
Mashabiki wa Kilimanjaro Stars inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, wakishangilia wakati wa mchezo wa Robo Fainali ya kwanza ya michunao ya Cecafa Challenge dhidi Rwanda uliochezwa katika Uwanja wa KCC uliopo Lugogo nchini Uganda. 
Picha na Shaffih Dauda Blog

Half time: Kilimanjaro Stars 1-0 Rwanda

Dak 45: Dakika 2 za nyongeza kipindi cha kwanza bado mpira ni Kilimanjaro Star 1-0 Rwanda

Dak 38: Mrisho Ngassa nusura aseme na golikipa wa Amavubi, mpira unapita sentimeta chache toka kwenye mtambaa wa panya na inakuwa ahueni kwa wanyarwanda hapa.


Amri Kiemba anaipatia Kilimanjaro Stars bao la kwanza baada ya Mwinyi Kazimoto kutoa pasi nzuri sana hivyo Kilimanjaro Stars inaongoza kwa bao moja hapa 
Kipa wa Rwanda aliyelala chini akijitahidi kuokoa goli lililofungwa na Amri Kiemba baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Mwinyi Kazimoto ya kuwapita mabeki wa timu ya Rwanda.Picha na Shaffih Dauda Blog
 
Dak 33: Goal Kilimanjaro Stars 1-0 Rwanda 


Dak 30: Bado matokeo ni sifuri kwa bila 

 
Dak 15: Kilimanjaro Stars 0-0 Rwanda

Mchezo wa robo fainali Kilimanjaro Stars vs Amavubi umeanza 
Kilimanjaro Stars XI vs Rwanda: Kaseja, Nyoni, Maftah, Kapombe, Yondani, Kiemba, Abubakar, Domayo, Kazimoto, Ngassa, Bocco 

Benchi la Tanzania: B.Munishi, I.Rashid, C.Edward, Y.Singano, A.Idd, S.Msuva, S.Nditi, M.Samatta, T.Ulimwengu.

Kikosi cha RWANDA: J.CNdori, E.Bayisenge, I.Nshutiyamagara, J.Mbaraga, C.Tibingana, M.Rusheshangora, J.B Mugiraneza, H.Niyonzima, J.C Iranzi, D.Birori, T.Ntamuhanga.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top