Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Rehema Chalamila 'RAY C' akimshukuru Rais Kikwete kwa msaada wa matibabu. (Picha na Freddy Maro)
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Ray C (wa tatu kushoto), Mama yake mzazi Ray C Bibi Margareth Mtweve (kushoto) na Sarah Mtweve Dada yake Ray C

Mwanamuziki wa Kizazi Kipya Rehema Chalamila maarufu kama RAY C amemtembelea Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dare s Salaam na kumshukuru kwa msaada wa matibabu wakati alipokuwa mgonjwa hivi karibuni.

Rehema alifuatana na Mama yake Mzazi Margareth Mtweve na Dada yake Sarah Mtweve.
 
Ray C alimweleza Rais kuwa, afya yake imeimarika na kwamba muda si mrefu atarejea jukwaani kukonga nyoyo za mashabiki wake.

  Mama Mzazi wa Ray C amemshukuru Rais Kikwete kwa kuokoa maisha ya mwanawe na vilevile ametoa wito kwa watu wanaokusanya michango kwa ajili ya mwanaye waache kufanya hivyo kwa kuwa matibabu ya Ray  C yamegharamiwa na Rais Kikwete.