Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MBATIA:UMBEA UMECHOCHEA YALIYONIKUTA MTWARA

 MWENYEKITI wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia 
Kwa ufupi

Hatua hiyo ilifuatia baada ya baadhi ya wananchi kuamua kumrushia chupa tupu za maji, huku wakimfuata kabla ya kuizingira ofisi hiyo wakiimba nyimbo za kumshtumu kuwa ni mamluki.

....................
MWENYEKITI wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia amesema yaliyomkuta kwenye yake ziara mkoani Mtwara ambako amelazimika kuikatisha, yametokana na umbea aliouita ni wa mwaka 2013.

Mbatia ambaye pia ni Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, alisema hayo jana kwenye Ofisi za Bunge Dar es Salaam.

“Unasemaje (anamuuliza mwandishi), ngoja nikwambie kilichotokea kimetokana na umbea tu wa mwaka mpya 2013, wewe tambua hivyo na sitazungumza lingine zaidi,” alijibu kwa kifupi akionyesha kukwepa kulizungumzia suala hilo zaidi.

Baadhi ya vyombo vya habari nchini viliripoti kuhusu Mbatia akiwa na wabunge wa chama chake, Moses Machali (Kasulu Mjini ) na Agripina Buyogela (Kasulu Vijijini) walilazimika kujifungia ndani ya ofisi za NCCR- Mageuzi wilayani Mtwara Mjini.


Hatua hiyo ilifuatia baada ya baadhi ya wananchi kuamua kumrushia chupa tupu za maji, huku wakimfuata kabla ya kuizingira ofisi hiyo wakiimba nyimbo za kumshtumu kuwa ni mamluki.

Ilielezwa kuwa, hali ilikuwa tete eneo la ofisi hiyo hasa baada ya giza kuingia, kwani wananchi walianza kurusha mawe juu ya ofisi hiyo na wengine kujaribu kuvunja mlango na kurusha vitu vinavyodiwa kuwa ni baruti zinazotumika kuvulia samaki .

Hali hiyo ilisababisha polisi waliofika kumuokoa kutumia mabomu ya machozi.
Mapema mwaka huu baadhi ya wananchi wa Mtwara waliandamana wakipinga gesi kusafirishwa kuletwa Dar es Salaam.
Badala yake, walitaka mtambo wa kuzalisha umeme kujengwa mkoani humo.


CHANZO:MWANANCHI
 
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top