Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MWAKYEMBE:MARUFUKU UOSHAJI MAGARI KATIKATI YA MJI

Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe, ameuagiza uongozi wa Mamlaka ya mji wa Kyela kupiga marufuku uoshaji magari katikati ya mji.
Dk. Mwakyembe alitoa agizo hilo jana baada ya kufanya ziara mjini hapa na kukuta vijana wakiosha magari pembeni mwa barabara karibu na Hospitali ya Wilaya.
Alichukua hatua hiyo baada ya kuhudhuria kikao cha madiwani wa Kamati ya Fedha na Uchumi ambacho pamoja na mambo mengine madiwani walijadili suala la tabia ya vijana kuosha magari katikati ya mji hali ambayo imekuwa ikisababisha uchafu wa mazingira.
Katika kikao hicho, Mtendaji wa Mamlaka ya Mji wa Kyela, Raphael Samwel, alisema vijana walikwisha elezwa wasitishe uoshaji magari katikati ya mji lakini hata hivyo bado wamekaidi agizo hilo hali ambayo imekuwa ikileta usumbufu kwa wananchi wengine.
Samwel alisema kutokana na hali hiyo wananchi ambao nyumba zao zipo karibu na maeneo kunapooshwa magari wamekuwa wakilalamika kutokana na uchafuzi wa mazingira unaofanywa na waosha magari hao.
Kufuatia hali hiyo, Dk. Mwakyembe alisema kuanzia sasa Mamlaka ya Mji wa Kyela ipige marufuku uoshaji wa magari katikati ya mji.
Alisema magari yote yawe yanaoshwa eneo la Bwawani na kuagiza viongozi wa Mamlaka ya Mji wa Kyela kupeleka huduma ya maji katika eneo hilo.
Alisema kwa upande atahakikisha anatengeneza banda kwa ajili kupumzika watu watakaokuwa wanasubiri wakati magari yao yanaoshwa.  

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top