Kwa ufupi
“Tunataka uchaguzi mdogo ufanyike katika kata hizi
kulingana na matakwa ya sheria. Tushinde Chadema, CCM, TLP, NCCR-Mageuzi
au CUF sawa. Muhimu wananchi wapate haki ya uwakilishi kwenye vikao vya
baraza la madiwani,” alisisitiza Mbowe.
...........
...........
Kata za Kimandolu, Themi, Kaloleni na Elerai ziko
wazi tangu Agosti 7, mwaka juzi baada ya waliokuwa madiwani, Estomih
Malla, Reuben Ngowi, Charles Mpanda na John Bayo na wa viti maalum,
Rehema Mohamed kufukuzwa uanachama wa Chadema kwa kosa la kukaidi
maagizo ya kamati kuu kuhusu mwafaka wa mgogoro wa Umeya.
Kata ya Sombetini yenyewe iko wazi baada ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo, Alphonce Mawazo kuhamia Chadema akitoka CCM.
Mbowe alisema chama chake kitachukua mkondo wa
shinikizo kwa Serikali na NEC baada ya kubaini mbinu za kuchelewesha
makusudi uchaguzi katika kata hizo kwa kile kinachoaminiwa ni hofu ya
CCM kuwa kata hizo zitatwaliwa na Chadema.
Akizungumza Arusha jana, wakati wa hafla fupi ya
kupokea hati za kiwanja chenye ukubwa wa hekari tatu kutoka kwa Kampuni
ya Mawala Trust kwa ajili ya ujenzi wa hospitali maalumu ya Mama na
Mtoto, Mbowe alisema wananchi wa kata hizo wana haki ya uwakilishi na
Chadema itawasaidia kuidai.
Alisema chama chake pia kitaendesha kampeni ya
kudai uchaguzi mdogo Sengerema na Buchosa alikosema pia kuna kata ziko
wazi baada ya waliokuwa madiwani kupitia tiketi ya CCM kuhamia Chadema
zaidi ya mwaka mmoja uliyopita.
“Tunataka uchaguzi mdogo ufanyike katika kata hizi
kulingana na matakwa ya sheria. Tushinde Chadema, CCM, TLP,
NCCR-Mageuzi au CUF sawa. Muhimu wananchi wapate haki ya uwakilishi
kwenye vikao vya baraza la madiwani,” alisisitiza Mbowe.
Baada ya kuvuliwa uanachama, Mallah na wenzake
wanne walifungua kesi kupinga uamuzi huo katika mahakama ya hakimu mkazi
Arusha, ambapo walishindwa na kukata rufaa Mahakama Kuu kabla ya kuamua
kuifuta kwa hiari Septemba 5, mwaka huu.
Waliokuwa madiwani hao ambao walikuwa wakitetewa
na Wakili Severin Lawena, hivi sasa wameamriwa kuilipa Chadema fidia ya
zaidi ya Sh15 milioni, baada ya Hakimu Mfawidhi, Charles Magessa
kukubaliana na ombi la madai yaliyowasilishwa na Wakili Method
Kimomogoro anayekiwakilisha Chadema na Mbowe aliyekuwa mdaiwa wa pili
katika kesi ya msingi.
NA MWANANCHI
NA MWANANCHI
Post a Comment