Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

LIVE MATCH CENTRE:TAIFA STARS 1-0 CAMEROON

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, imelaza timu ya taifa ya cameroun yenye wachezaji wenye mvuto mkubwa na misuli iliyokwenda shule labda mcheza wa Totenham unaweza kumuita mchakarikaji mkubwa, akihaha uwanja mzima katika kusaka ushindi lakini alikuwa Samata aliyewaua leo.



................. 
DDk 90 FULL TIME! Taifa Stars 1-0 Cameroon.

Dk 89 Goooo..! Mbwana Samatta anaifungia Taifa Stars bao la kuongoza akiunganisha krosi ya Erasto Nyoni.

Dk 85 Cameroon inafanya mabadiliko wametoka Aboubakar Vincent na Bouba wameingia Bakinde Gerard na Makoun Jean.

Dk 83 Amri Kiemba wa Taifa Stars anakosa bao la wazi bao la wazi baada ya mpira aliokuwa akiusubiri kuingiliwa na beki wa Cameroon, Assou Ekotto.

Dk 79 Kaseja anadaka shuti kali la Ashu Clovis wa Cameroon. Walikuwa wamebaki wawili tu.

Dk 73 Cameroon inafanya mabadiliko anatoka Bedimo Henri anaingia Ashu Clovis.

Dk 70 Sure Boy anapiga shuti kali langoni kwa Cameroon lakini beki Ngoula anautoa nje na kuwa kona butu.

Dk 68 Cameroon inafanya mabadiliko anatoka Olinga Fabrice anaingia Edoa Charle.

Dk 66 Sure Boy anapiga shuti kali katika lango la Cameroon lakini kipa Effala Komguep anadaka.

Dk 60 beki wa Cameroon Aminou Bouba anabanwa misuli na kutibiwa uwanjani wakati Taifa Stars ikiwa katika shambulizi kali.

Dk 60 beki wa Cameroon Aminou Bouba anabanwa misuli na kutibiwa uwanjani wakati Taifa Stars ikiwa katika shambulizi kali.

Dk 58 Cameroon inafanya mabadiliko anatoka Tchami Herve anaingia Eloundu.

Dk 56 Taifa Stars inafanya mabadiliko anatoka Mwinyi Kazimoto anaingia Thomas Ulimwengu.

Dk 54 Ngoula wa Cameroon anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Mrisho Ngassa.

Dk 48 Taifa Stars inafanya shambulizi kali langoni kwa Camerooni.

Dk 48 Taifa Stars inafanya shambulizi kali langoni kwa Camerooni.

Dk 45 Kipindi cha pili kimeanza
 

kipindi cha pili fuatilia hapa https://www.facebook.com/Rundugaiblog?ref=ts&fref=ts
HT: Taifa Stars 0-0 Cameroon

Ngassa aliichambua defense ya Cameroon na kubaki yeye na kipa tu lakini shuti lake linaokolewa na matokeo ni bila kwa bila mpaka sasa.

Dk 30: Taifa Stars 0-0 Cameroon

Dk 28 Erasto Nyoni anakosa penati kwa upande wa Stars hivyo Taifa Stars 0-0 Cameroon
 
Dk 27 Stars inapata penati

Dk 20:Nahodha Juma Kaseja anapatiwa matibabu uwanjani baada ya kuumizwa wakati akiokoa hatari langoni 

Dk 18: Kadi ya njano kwa Frank Domayo
Dk 17: Taifa Stars 0-0 Cameroon

DK 02:Taifa Stars 0-0 Cameroon
LINE UP: TAIFA STARS, Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Kelvin Yondan, Aggrey Morris, Salum Aboubakar 'Sure Boy', Mrisho Ngassa, Frank Domayo, Mbwana Samatta, Mwinyi Kazimoto na Amri Kiemba

CAMEROON: Effala komguep,assou ekotto,aminou bouba,ngoula,nyom allan,pierre wome nlend,kingue mpondo,bedimo henry,tchami herve,olinga fabrice,aboubak vicent.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top