Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MELI YA MV VICTORIA YANUSURIKA KUTEKETEA KWA MOTO

HABARI kutoka Jijini Mwanza kupitia G Sengo tunataarifiwa kuwa...
 
MELI ya Mv Victoria inayomilikiwa na Kampuni ya huduma za Meli nchini(MSC)imenusurika kuteketea kwa moto uliozuka wakati mafundi wa kampuni hiyo wakichomelea sehemu mojawapo ya Meli hiyo.

Moto huo uliozuka katika meli hiyo ulizua tafrani kwa wakazi wa jiji la Mwanza na kufurika katika eneo la maegesho ya Meli za Kampuni ya MSC yaliyopo katika bandari ya Mwanza kaskazini majira ya saa 8 na dakika kadhaa na kusababisha msongamano mkubwa katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa taarifa zlizo patikana toka kwa wafanyakazi wa Meli hiyo zimeleeza kuwa maundi wa kampuni walikuwa wakichomelea katika moja ya vyumba vya chini vya Meli hiyo ndipo cheche za moto ulipoangukia katika sehemu ya kuhifadhia mizigo na kuanza kuwaka.

Sehemu hiyo ya mizigo kulikuwa kumehifadhiwa magodoro pamoja na mito ya makochi tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenda mjini Bukoba Mkoani Kagera leo usiku.

Hata hivyo moto huo uliodumu kwa takribani nusu uliokuwa ukiwaka toka katika chumba cha kuhifadhia mizigo kilichopo sehemu ya chini ya Meli ya Mv Victoria ulidhibitiwa na kikosi cha zima moto na uokoaji waliowasili katika eneo hilo mudamchache baada ya moto kuanza wakitumia gari lenye namba z ausajili STK 1965 Mali ya Halmashauri ya jiji la Mwanza.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top