Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

PUNGUZO LA KODI KWA WAFANYAKAZI KIINI MACHO


 Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa akiingia bungeni Dodoma jana kusoma hotuba ya Bajeti. Picha na Fidelis Felix.
Kwa ufupi
.........
Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, viwango vinavyopendekezwa ni ikiwa mfanyakazi anapata jumla ya mapato yasiyozidi Sh2,040,000 kwa mwaka ambayo ni sawa na Sh170,000 kwa mwezi, kiwango cha kodi ni asilimia 0, kwa maana kwamba hatalipa kodi.
,,,,,,,,
Dar es Salaam. Bajeti ya Serikali ya mwaka 2013/14 inaonyesha kuwa wafanyakazi wamepunguziwa kodi katika mishahara yao ingawa punguzo lenyewe linaonekana kama kiini macho.
Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali bungeni Dodoma jana, Waziri wa Fedha, William Mgimwa alisema Serikali imependekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Kodi ya Mapato ili kupunguza kodi hiyo.
Waziri Mgimwa alisema Serikali imepunguza kiwango cha chini cha kutoza kodi ya mapato ya ajira kutoka asilimia 14 hadi 13... “Hatua hii inalenga katika kutoa nafuu ya kodi kwa mfanyakazi.”
Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, viwango vinavyopendekezwa ni ikiwa mfanyakazi anapata jumla ya mapato yasiyozidi Sh2,040,000 kwa mwaka ambayo ni sawa na Sh170,000 kwa mwezi, kiwango cha kodi ni asilimia 0, kwa maana kwamba hatalipa kodi.
Kwa wafanyakazi wenye mapato ya jumla yanayozidi Sh2,040,000 lakini hayazidi Sh4,320,000 sawa na Sh360,000 kwa mwezi kiwango cha kodi atakachokatwa ni asilimia 13 baada ya malipo ya Mfuko wa Jamii ambayo ni nafuu ya isiyozidi Sh1,540.
Kwa wafanyakazi wenye mapato yanayozidi Sh361,000 kuendelea watapata nafuu ya Sh1,900.
MISHAHARA KIMYA
Dk Mgimwa hakuzungumzia suala lolote kuhusu kupandishwa kwa mishahara tofauti na kilio cha Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), ambalo katika sherehe za Mei Mosi, mwaka huu zilizofanyika kitaifa mkoani Mbeya, lilipendekeza kima cha chini cha mshahara kiwe Sh740,000 kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

MWANANCHI
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top