|
Meneja
Mkuu wa Kampuni ya ufyatuaji matofali ya Ujenzi Solutions, ya Kimara
kwa Msuguri, Dar es Salaam, Rahim Hamis na mfanyabiashara wa kampuni
isiyo na jina, Credo Rajab (kulia) wakiwa chini ya uliznzi wa Polisi
huku wakiwa wamevishwa pingu baada Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla
kuamuru kuwakamata alipokagua viwanda vyao vya ufyatuaji na kugundulika
kuwa wanatumia maji isivyo halali kwa kujiunganishia kwenye bomba kuu la
Mamlaka ya Maji Safi na Taka Dar ws Salaam (DAWASA). Makalla ambaye
alifanya ziara ya kukagua maendeleo ya upanuzi wa Matambo wa Maji wa
Ruvu Juu, Mlandizi, mkoani Pwani , pia alifanya msako wa kushitukiza kwa
kampuni hizo. |
|
Naibu
Waziri wa Maji, Amos Makalla (kulia) akijaribu kuendesha katapila la
Kampuni ya Ujenzi ya VA Tech Wabag Ltd, alipofanya ziara ya kukagua
maendeleo ya upanuzi wa Mitambo ya Maji ya Ruvu Juu, Mlandizi, mkoani
Pwani .Katikati ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini, Hamoud Jumaa na
Meneja Mradi wa kampuni hiyo, Pintu Dutta. |
|
Askari wa FFU wakilinda doria katika kiwanda cha ufatuaji tofali cha Ujenzi Solutions, Kimara Dar es Salaam |
|
Moja
ya mabomba linalodaiwa kuunganishwa kiholela kwenye bomba kuu la Ruvu
Juu linaloleta maji mjini na kampuni ya Ujenzi Solutions eneo la Kimara |
|
Makalla
akizungumza mbele ya Lori la Maji lililokamatwa likijazwa maji
yanayodaiwa kuwa ya Dawass, katika kiwanda cha matofali cha Ujenzi
Solutions |
|
Pumpu iliyonaswa na Dawasa ikinyonyonya maji kutoka bomba kuu la Ruvu Juu eneo la Ubungo, Dar es Salaam |
|
Makalla
akiondoka katika kiwanda cha matofali cha Moto ambacho alisitisha
shguli zake baada ya kubainika wakiiba maji ya Dawasa eneo la Ubungo. |
|
Ramani ya upanuzi wa Mtambo wa Maji wa Ruvu Juu, eneo la Mlandizi, Pwanik. |
|
Mbunge
wa Jimbo la Kibaha Vijijini, Hamoud Jumaa akijaribu kuendesha katapila
la Kampuni ya Wagani ambayo imepewa tenda ya upanuzi wa Mtambo wa Maji
wa Ruvu Juu. |
Makalla
(wa pili kushoto) Mbunge wa Kihaha Vijijini, Hamoud Jumaa ( wa pili
kulia) na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Halima Kihemba kulia, wakikagua
ujenzi wa upanuzi wa mtambo huo. PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG
This post was written by: Author Name
Your description comes here!
Get Free Email Updates to your Inbox!
Filed Under:
Jamii
on Tuesday, July 15, 2014
Post a Comment