Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TB JOSHUA KUSHUHUDIA KUAPISHWA KWA RAIS DR MAGUFULI

Dkt Magufuli ampokea TB Joshua Uwanja wa ndege Dar jioni hii. Mhubiri huyo aliyekuja na watu 40 kwa ndege yake mwenyewe, amekuja kushuhudia Dkt Magufuli akiapishwa
 ( Picha na Ikulu)

Na Mwandishi WETU Dar 
Mtume TB Joshua wa Kanisa la Church of All Nations la nchini Nigeria, ametua Jijini Dar es Salaam leo, kwa ajili ya kuja kushuhudia kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya Tano Dk. John Pombe Magufuli.

Mara baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, TB Joshua alikwenda moja kwa moja Ikulu, kumsalimia Rais Jakaya Kikwete.

Katika mazungumzo yao, TB Joshua alimpongeza Rais Kikwete kwa kufanikisha uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani, uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu, ambao alisema ulifanyika kwa uhuru na amani.
Alimweleza Rais Kikwete kuwa, kutokana na kufanikisha uchaguzi huo, anaondoka madarakani kwa furaha na amani.
Aidha, alimpongeza Rais Kikwete kwa kukiwezesha Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumpata Dk. Magufuli kuwa raia wa awamu ya tano.
Alimwelezea Dk. Magufuli kuwa ni Rais wa Baraka na Fanaka tele katika awamu hii mpya.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top