Dkt
Magufuli ampokea TB Joshua Uwanja wa ndege Dar jioni hii. Mhubiri huyo
aliyekuja na watu 40 kwa ndege yake mwenyewe, amekuja kushuhudia Dkt
Magufuli akiapishwa
( Picha na Ikulu)
Na Mwandishi WETU Dar
Mtume
TB Joshua wa Kanisa la Church of All Nations la nchini Nigeria, ametua
Jijini Dar es Salaam leo, kwa ajili ya kuja kushuhudia kuapishwa kwa
Rais wa Awamu ya Tano Dk. John Pombe Magufuli.
Mara
baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,
Dar es Salaam, TB Joshua alikwenda moja kwa moja Ikulu, kumsalimia Rais
Jakaya Kikwete.
Katika
mazungumzo yao, TB Joshua alimpongeza Rais Kikwete kwa kufanikisha
uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani, uliofanyika Oktoba 25, mwaka
huu, ambao alisema ulifanyika kwa uhuru na amani.
Alimweleza Rais Kikwete kuwa, kutokana na kufanikisha uchaguzi huo, anaondoka madarakani kwa furaha na amani.
Aidha, alimpongeza Rais Kikwete kwa kukiwezesha Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumpata Dk. Magufuli kuwa raia wa awamu ya tano.
Alimwelezea Dk. Magufuli kuwa ni Rais wa Baraka na Fanaka tele katika awamu hii mpya.
Post a Comment