Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje aongoza maadhimisho ya miaka 44 ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE)

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya miaka 44 ya  Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) zilizofanyika kwenye Ubalozi wa UAE hapa nchini hivi karibuni. Katika hotuba yake Balozi Yahya alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na UAE ili kujiletea maendeleo.
Sehemu ya Mabalozi na Wageni waalikwa walioshiriki maadhimisho ya miaka 44 ya UAE
Balozi wa UAE hapa nchini, Mhe.Abdulla Ibrahim Alsuwaidi nae akitoa hotuba wakati wa maadhimisho hayo ambapo aliisifu Tanzania kuwa ni nchi inayoshirikiana kwa karibu na UAE katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Abdallah Kilima akiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara hiyo, Bi. Mindi Kasiga (katikati) pamoja na wageni wengine waalikwa wakifuatilia hotuba ya Balozi Alsuwaidi (hayupo pichani).
Balozi Yahya kwa pamoja na Balozi Alsuwaidi na Mabalozi wengine wakikata keki kuashiria maadhimisho ya miaka 44 ya UAE
Balozi Yahya na Balozi Alsuwaidi wakimkabidhi tiketi ya ndege ya shirika la Emirates Afisa kutoka Ubalozi wa Msumbiji alipojishindia tiketi hiyo katika droo iliyoendeshwa kusherekea miaka 44 ya uhuru wa UAE
Balozi Yahya nae akifurahia tiketi ya Ndege ya Shirika la ETIHAD baada ya kushinda bahati nasibu katika halfa hiyo. Shirika hilo kutoka UAE limezindua safari zake hapa nchini tarehe 01 Desemba, 2015
Kiongozi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa DRC, Mhe. Juma Halfan Mpango nae akifurahia zawadi aliyojishindia
Mtoto mdogo aliyeshiriki maadhimisho hayo ni mmoja kati ya wale waliojishindia tiketi ya Ndege ya Shirika la ETIHAD

Balozi Kilima akiwa na Bw. Seif Kamtunda, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia matukio
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Hangi Mgaka nae akifuatilia matukio wakati wa maadhimisho ya UAE.

.............Matukio mengine kwenye maadhimisho ya miaka 44 ya UAE






























Balozi Abdulla Ibrihim Alsuwaidi akimpokea Balozi Yahya alipowasili Ubalozini hapo kabla ya kuanza maadhimisho ya miaka 44
Balozi Alsuwaidi akimpokea Balozi Abdallah
Balozi Alsuwaidi akimkaribisha Balozi wa Uganda hapa nchini
Balozi Alsuwaidi akimkaribisha Balozi wa Vatican hapa nchini
Bi. Mindi akibadilishana mawazo na mmoja wa wageni waalikwa wakati wa maadhimisho ya miaka 44 ya UAE
Bw. Omar Mjenga (kushoto) kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nae akiwa kwenye maadhimisho hayo.
Wageni waalikwa


Bi. Ester Baruti (kulia), Mwakilishi wa Kampuni ya Dangote hapa nchini akishiriki maadhimisho ya UAE


=======================
Picha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top