Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

PPF YAIBUKA KIDEDE KATIKA UTUNZAJI BORA WA HESABU ZAKE, YATWAA TUZO YA WA HESABU UPANDE WA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII



Na K-Vis Media/Khalfan Said.
MFUKO wa Pensheni wa PPF, umeibuka kidedea kwa kutwaa tuzo ya uwasilishaji bora wa hesabu zake katika kipindi cha mwaka 2014.

Katika hafla ya kutoa tuzo kwa taasisi za serikali na za watu binafsi, Bodi ya Taifa ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu, NBAA, imetoa tuzo hizo kwa makampuni na taasisi mbalimbali nchini, ambapo kwa upande wa kundi la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, PPF ndiyo iliibuka ya kwanza ambapo Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko huo, Bw. Martin Mmari kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu Bw. William Erio, alipokea tuzo hiyo kutoka kwa mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Khamis Mwinyimvua. Pichani Bw. Mmari akipokea tuzo hiyo kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bw. Khamisi Mwinyimvua. 
(Picha na K-Vis Media/Khalfan Said)
Bw. Khamisi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na umuhimu wa kuwasilisha taarifa sahihi za hesabu.
Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. Martin Mmari, (katikati), akiwa amekamata tuzo wakati wa kupiga picha na baadhi ya wafanyakazi wa Mfuko huo kwenye hafla ya kutolewa tuzo ya taasisi iliyowasilisha taarifa za mahesabu za mwaka 2014 kwa kuzingatia taratibu na kanuni za mahesabu kwenye kituo cha mikutano cha Bodi ya Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu NBAA, huko Bunju nje kidoto ya jiji la Dar es Salaam, Desemba 5, 2015. PPF ilishika nafasi ya kwanza katika kundi la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Tuzo hizo hutolewa na NBAA
Bw. Mamri (wapili kulia), akigongesha glasi na mmoja wa waalikwa wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya wawakilishi wa PPF katika hafla hiyo.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top