Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Temeke yajipanga kukabiliana na mangonjwa ya milipuko.

Uongozi wa manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam umeanza kujipanga ili kukabiliana na uwepo wa magonjwa ya milipuko kama kipindupindu ambapo umeanza harakati za kutoa elimu ya usafi kwa wananchi.


Akizungumza na ITV baada ya kutia saini mkataba wa sh bilioni 1.3 kati ya manispaa hiyo na taasisi ya Water AID, mkuu wa wilaya hiyo Bi Sophia Mjema amesema lengo ni hakuhakikisha manispaa hiyo inakuwa ya mfano kwa Tanzania kwa usafi huku akitoa onyo kali kwa watu wanaofanya uchafuzi wa mazingira.
 
 
Aidha mkurugenzi wa manispaa Temeke Bwana Fortdas amesema      atahakikisha fedha hizo zinatumika kwa lengo lililokusudiwa na si vinginevyo.
 
 
Naye mkurugenzi mtendaji wa shirika la Aater AIDS amesema lengo kuu la msaada huyo ni kuhakiksha watu wanaishi kwenye mazingira safi na salama pia kupata ajira kupitia mradi huo.
 
ITV
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top