Rais
mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ametunukiwa
Shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa ya mahusiano ya kimataifa jana
Jijini Dar es Salaam katika mahafaliya 30 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania.
Mhe.
Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema amefarijika sana kutunukiwa Shahada
hiyo ya heshima itolewayo na Chuo kikuu Huria Tanzania kwa watu ambao
wametoa mchango katika maendeleo katika jamii kupitia nafasi zao
kiutendaji.
“Naipokea
heshima hii toka Chuo Kikuu Huria Tanzania kwa moyo mmoja kwani wameona
mchango ambao nimeutoa nilipokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kwa Awamu ya Nne hivyo basi nitaendeleza mahusiano na
ushirikiano kimataifa”.Alisema Mhe. Dkt Kikwete.
Mbali
na Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kuna baadhi ya maraisi na wakuu mbalimbali
duniani waliwahi kupata Shahada za heshima toka Chuo Kikuu Huria
Tanzania ambao ni Rais wa Awamu ya Kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere, Rais wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais
wa Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa, Rais wa zamani wa Afrika ya
Kusini Hayati Nelson Mandela na Dkt Koichiro Mastuura Mkurugenz iwa
UNESCO.
Chuo
kikuu Huria cha Tanzania kimetoa jumla ya wahitimu 69 wawili Shahada
maalum na 67 ni Shahada, Stahahada na Astashahada, ambapo Shahada ya
uzamivu ni wahitimu watatu, Shahada ya uzamili ni wahitimu 20, Shahada
wahitimu 22,Stashahada wahitimu 15 na Astashahada wahitimu 6.
Tangu
kuanzishwa kwa Chuo Kikuu Huria Tanzania mwaka 1992 jumla ya wahitimu
25,908 wametunukiwa Shahada mbalimbali na haya ni mahafali ya 30 tangu
chuo kuanzishwa
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Dkt Asha Rose
Migiro akimpongeza Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete baada
ya kumtunuku Shahada ya heshima ya udaktari
wa falsafa ya mahusiano ya kimataifa katika maafali ya 30 ya Chuo kikuu Huria Tanzania
yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.
Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho
Kikwete akiongea na wanataaluma na wageni katika maafali ya 30 ya Chuo kikuu Huria Tanzania
yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Dkt Asha Rose
Migiro akifungua rasmi mahafali ya 30 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania
yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Chuo Kikuu
Huria cha Tanzania (OUT), Dk.
Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu,
Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika ana,
Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi ya
Kinondoni, Dar es Salaam. (Picha zote na Bashir Nkoromo-CCM Blog)
Mkuu wa Chuo Kikuu
Huria cha Tanzania (OUT), Dk.
Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu,
Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo,
Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi ya
Kinondoni, Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari ya
Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya
Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo,
Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi ya Kinondoni, Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu
Huria cha Tanzania (OUT), Dk.
Asha Rose Migiro akimpongeza baada ya kumhudhurisha Shahada ya heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu,
Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo,
Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi ya
Kinondoni, Dar es Salaam.
Dk. Kikwete akishukuru
Dk. Kikwete akingoka baada ya kuhudhurishwa
Dk.
Kikwete akiwa na Rais wa Chuo Kikuu cha Choson cha Korea, Profesa Such
Chae Hong, ambaye naye pia alitunukiwa Shahada ya heshima ya Udaktari
katika Mahahali hayo
Dk.
Kikwete na Profesa Such wakiwa wamesimama kuimba wimbo wa Taifa baada
ya kutunukiwa Shahada zao za Udaktari. Kulia ni Mkuu wa Chuo Kikuu Huria
cha Tanzania, Dk. Asha-Rose Migiro
Dk. Kikwete na Profesa Such na Mama Salma Kikwete wakiwa na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dk. Asha-Rose Migiro
Dk.
Kikwete na Profesa Such wakiwa Dk. Asha-Rose Migiro na viongozi wengie
wa Chuo Kikuu Huria. Karibu na Dk. Migiro ni Rais Mstaafu, Ali Hassan
Mwinyi
Dk. Kikwete na Profesa Such wakiwa na Mama salma Kiwete na Dk. Asha-Rose Migiro na baadhi ya viongozi wa OUT
Mama Salma Kikwete akiteta jambo na Dk. Asha-Rose Migiro
Dk. Jakaya Kikwete akimpongeza mmoja wa wahitimu katika chuo hicho mwenye ulemavu wa miguu.
Dk.
Jakaya Kikwete akimdodosa maswali, mtoto Novatus Salala (11), ambaye
alimuona akimpiga picha kwa simu wakati wa mahafali hayo. Kulia ni Mama
Salma Kikwete
Dk.
Jakaya Kikwete akiwa na Mkuu wa Chuo Kikuu huria w zamani, Dk. John
Malecela na Mkuu wa sasa wa Chuo hicho, Dk. Asha-Rose Migiri wakati
akiondoka mwishoni mwa hafla hiyo.
Post a Comment