Na Jumbe Ismaill, Singida
NAIBU
Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto amesema
asilimia 15 ya wanawake wamegundulika kuwa wamekeketwa na kwamba takwimu
hizo zinaonyesha pia kuwa ukeketaji huo umekithiri katika mikoa minane
hapa nchini.
Naibu
Waziri huyo,Dk.Hamisi Kigwangala ametoa takwimu hizo alipokuwa akifunga
kongamano la siku ya kupinga vitendo vya ukeketaji dhidi ya watoto wa
kike na wanawake lililofanyika mjini hapa.
Alifafanua
naibu waziri huyo kuwa takwimu hizo zinaonyesha kwamba ukeketaji huo
umekithiri katika mikoa ya Manyara,Dodoma,Arusha,Singida pamoja na mkoa
wa Mara na kwamba ukubwa wa tatizo hilo katika mikoa hiyo linatokana na
imani na mila potofu.
“Kwa
mujibu wa utafiti wa kidemografia na Afya Tanzania (Tanzania
Demographic and Health Survey) wa mwaka 2010 unaonyesha kuwa asilimia 15
ya wanawake wamekeketwa na kwamba takwimu hizo zinaonyesha ukeketaji
umekithiri katika mikoa ya Manyara asilimia 71”alisema.
Aliitaja
mikoa na asilimia zake kuwa ni mkoa wa Dodoma asilimia 64,Arusha
asilimia 59,Singida asilimia 51 na Mara asilimia 40 huku akiweka bayana
kuwa takwimu hizo zinaonyesha pia ukubwa wa tatizzo la ukeketaji katika
mikoa ya Dar-es-Salaam,Morogoro na Pwani kutokana na watu wa makabila
mbali mbali kuhamia katika mikoa hiyo.
“Serikali
inapinga,kulaani na kukemea tabia ya kuendelezwa kwa vitendo hivi vya
ukatili unaomdhalilisha mtoto wa kike kwani unamsababishia madhara
makubwa kiafya,kielimu, kisaikolojia na kimaendeleo”alisisitiza
Dk.Kigwangala.
Katika
kuhakikisha kuwa suala la udhalilishaji kwa wanawake na watoto wa kike
linazuiwa na kutokomezwa kabisa nchini,Dk.Kigwangala alibainisha kuwa
serikali imesaini na kuridhia mikataba ya kimataifa na kikanda,maazimio
na makubaliano mbali mbali yanayohusu haki na maendeleo ya watoto na
wanawake.
Hata
hivyo Naibu waziri huyo aliitaja baadhi ya mikataba hiyo kuwa ni pamoja
na mkataba wa kimataifa wa Haki za mtoto wa mwaka 1989,Mkataba wa
kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake wa mwaka 1989,mkataba wa
Afrika wa Haki za Binadamu na Haki za watu wa mwaka 1982 na itifaki yake
ya nyongeza inayohusu wanawake wa Afrika wa mwaka 2003 inayopinga mila
zenye kuleta madhara kwa binadamu kama vile ukeketaji.
Akitoa
salamu za shukurani mara baada ya hotuba ya mgeni huyo,Mkurugenzi
Mtendaji wa TAMWA,Edda Sanga aliweka wazi kwamba suala la harakati za
ukeketaji ni harakati ambazo zimeweza kuleta machungu mengi katika
jamii,jambo ambalo linahitaji msukumu mkubwa wa serikali.
Kwa
mujibu wa Mkurugenzi huyo licha ya machungu yanayotokana na vitendo vya
ukeketaji kunakosababisha vilio vya watu kutoka sehemu
mbalimbali,lakini vilio peke yake havitasaidia chochote na kwamba ni
wakati muafaka sasa wa kuchukua hatua za kuhakikisha mila na desturi
zilizopitwa na wakati zinatoweka kabisa nchini.
“Mheshimiwa
Naibu waziri tulilia hapa machozi jana lakini kama unavyojua mheshimiwa
waziri machozi hayatoshi ni lazima tuchukua hatua na hatua ndizo hizo
ambazo umetuahidi hapa,jamani naomba tumpigie makofi mheshimiwa
waziri”alisisitiza Sanga.
baadhi
ya wanaharakati wa mapambano dhidi ya kupinga vitndo vya ukeketaji
kutoka katika mikoa mitano ya Tanzania Bara waliohudhuria kongamano la
siku mbili lililofaanyika mjini Singida.
Post a Comment