Wachezaji
wa timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamezawadiwa
magari ya kifahari baada ya kushinda Kombe la Taifa Bingwa Afrika kwa
wachezaji wa ligi za nyumbani (CHAN).Rais Joseph Kabila amemtunuku kila mchezaji gari gari la kifahari la thamani ya $60,000 (£40,000).Wachezaji hao pia wamepewa nishani.Wachezaji wa DR Congo walakiwa kishujaa
Chui hao wa Kinshasa walitwaa kombe kwa kulaza Mali 3-0 kwenye fainali na kuwa taifa la kwanza kushinda kombe hilo mara mbili
Mwandishi
wa BBC Mbelechi Msochi anasema mchezaji Heritier Luvumbu Nzinga
aliyeumia kwenye michuano hiyo pia ameahidiwa kwamba atasafirishwa
ng'ambo kwa matibabu.
Post a Comment