Mh:Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Ndg,Mwigulu Lameck Nchemba akiwasili kata ya Hembeti,Kijiji cha Dihinda mapema hii leo kuangalia madhara na kuchukua hatua dhidi ya uhusiano mbaya uliopo kati ya wakulima na wafugaji uliopelekea kuuawa kwa mbuzi Zaidi ya 70 kwa kukatwakatwa mapanga wilayani Mvomero.
Mh;Mwigulu Nchemba akizungumza na wananchi wa kata ya Hembeti wilaya ya Mvomero wakati wa hatua za awali za kutafuta suluhu ya kuondokana na mapigano ya wakulima nawafugaji yaliyosababisha Mbuzi zaidi ya 70 kukatwa katwa usiku wa kuamkia tar 9/02/2016 katika kitongoji cha Dihinda.
Katika Mkutano huo,Mwigulu pamoja na
wananchi wamekubaliana tar 21/02/2016 kutafanyika mkutano mkubwa utakao
husanisha wakulima na wafugaji ilikuweka mipaka ya kutenganisha eneo la
kufigia na kilimo.
Wakati huohuo wote walioshiriki kwenye
tukio la kukata kata mifugo wameshaanza kukatwa na kuchukuliwa hatua za
kisheria,Mwigulu amesisitiza kuwa si vyema kujenga tabia ya visasi baina
ya wakulima na wafugaji.Serikali imeshajipanga kuanza kugawa maeneo
kwaajili ya jamii hizi mbili katika sehemu mbalimbali za nchi,hivyo basi
wananchi wa Mvomero na sehemu zingine wawe wavumilivu wakati huu
serikali ikianza kugawa maeneo upya kwaajili ya hifadhi,kilimo na
malisho ya mifugo.
Mh:Mwigulu Nchemba akipokea baadhi ya maelezo kutoka kwa Mkuu wa polisi (RPC) Mkoa wa Morogoro kuhusiana na tukio la mapigano ya wakulima na wafugaji eneo la Mvomero.
Mama mjane akilia mbele ya mifugo yake iliyouawa kwa kukatwakatwa mapanga.
Mwigulu Nchemba akishuhudia madhara yaliyotokana na ugomvi wa wakulima na wafugaji kitongoji cha Dihinda uliopelekea mbuzi hawa kukatwakatwa.
Mwigulu Nchemba akiwa ameongozana na mama mjane aliyejeruhiwa na mbuzi wake kukatwa katwa mapanga na watu wanaodhaniwa ni wakulima katika kitongoji cha Dihinda.
Sehemu ya Mbuzi waliouawa kwa kukatwa katwa mapanga na watu wanaodhaniwa ni wakulima wilayani Mvomero.
Mwigulu akiwa na Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mh:Betty Mkwasa wakiangalia madhara yaliyosababishwa na uhusiano mbaya kati ya wakulima na wafugaji eneo la kata ya Hembeti.
Waziri wa Kilimo.Mifugo na Uvuvi Mh:Mwigulu Nchemba na Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mh:Betty Mkwasa wakichanja mbuga za kijiji cha kigurukirwa wakati wa kukagua madhara yaliyotokana na uhusiano mbaya kati ya wakulima nawafugaji wilayani mvomero hii leo.
Mh:Mwigulu Nchemba akipokea baadhi ya maelezo kutoka kwa Mkuu wa polisi (RPC) Mkoa wa Morogoro kuhusiana na tukio la mapigano ya wakulima na wafugaji eneo la Mvomero.
Mama mjane akilia mbele ya mifugo yake iliyouawa kwa kukatwakatwa mapanga.
Mwigulu Nchemba akishuhudia madhara yaliyotokana na ugomvi wa wakulima na wafugaji kitongoji cha Dihinda uliopelekea mbuzi hawa kukatwakatwa.
Mwigulu Nchemba akiwa ameongozana na mama mjane aliyejeruhiwa na mbuzi wake kukatwa katwa mapanga na watu wanaodhaniwa ni wakulima katika kitongoji cha Dihinda.
Sehemu ya Mbuzi waliouawa kwa kukatwa katwa mapanga na watu wanaodhaniwa ni wakulima wilayani Mvomero.
Mwigulu akiwa na Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mh:Betty Mkwasa wakiangalia madhara yaliyosababishwa na uhusiano mbaya kati ya wakulima na wafugaji eneo la kata ya Hembeti.
Waziri wa Kilimo.Mifugo na Uvuvi Mh:Mwigulu Nchemba na Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mh:Betty Mkwasa wakichanja mbuga za kijiji cha kigurukirwa wakati wa kukagua madhara yaliyotokana na uhusiano mbaya kati ya wakulima nawafugaji wilayani mvomero hii leo.
Picha na Sanga Festo Jr.
Post a Comment