Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Watumishi wa Mambo ya Nje wapata somo kuhusu umuhimu wa Viwanda vidogo katika maendeleo ya nchi

 Meneja Mkuu wa Kampuni ya SG ya nchini India, Dkt. Pralay Dey akiwasilisha mada  kuhusu Role of SMEs in Industrialization: Lessons from India kwa Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Taasisi na Idara mbalimbali za Serikali (hawapo pichani), katika mhadhara huo uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam Dkt. Dey alieleza umuhimu wa Tanzania kuwa na mradi wa Mfano wa Uzalishaji wa Viwanda Vidogo "incubator" ili kufikia mapinduzi ya viwanda na kuwawezesha Watanzania kupata ajira.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto) pamoja na Naibu Balozi wa India, Bw. Robert, wakifuatilia mada kutoka kwa Dkt. Dey (hayupo pichani).

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katikaWizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Selestine Mushi akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo nchini (SIDO) Injinia Omary Bakari wakifuatilia mada.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa. Bi. Mindi Kasiga ambaye pia alikuwa mratibu na muongozaji wa Mdahalo naye akifuatilia mdahalo huo.

Mmoja wa washiriki wa mdahalo huo akichangia hoja.
Baadhi ya Maafisa kutoka Taasisi na Idara mbalimbali za Serikali walioshiriki Mhadhara ulioandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wakijadili jambo na mtoa mada mara baada ya kumaliza mhadhara huo.
Picha ya pamoja.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top