Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KONSELI MKUU WA TANZANIA JEDDAH AKARIBISHWA RASMI NA MKURUGENZI MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NJE YA SAUDI ARABIA, NAYE AMWALIKA KUTEMBELEA TANZANIA MWEZI JULAI 2016

Pichani Balozi Muhammad Tayeb, Mkurugenzi Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudi Arabia akimkaribisha Bw. Suleiman Saleh, Konseli Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jeddah, na kufanya nae mazungmzo kuhusu mahusiano baina ya Saudi Arabia na Tanzania.

Kwa mujibu wa Balozi Tayeb, kusainiwa kwa makubaliano hayo kumefungua ukurasa mpya wa mahusiano baina ya Saudi Arabia na Tanzania na hakusita kuonyesha furaha yake kutokana nakuainishwa maeneo mahususi ya mashirikiano  katika sekta za uchumi, uwekezaji na biashara. Kwa upande wake Bw. Saleh alimshukuru Balozi Muhammad Tayeb kwa kumkaribisha Ofisini kwake na alifarijika na upendo alionyesha Balozi huyo kwa Tanzania ambapo  alichukwa fursa hiyo kumualika kutembelea Tanzania kujionea vivutio vya utalii Tanzania Bara na Visiwani ambapo aliukubali mwaliko huo na kuahidi kutembelea Tanzania yeye na familia yake mwezi Julai, 2016.

========================================

Konseli Mkuu wa Ubalozi Mdogo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliopo Jeddah, Saudi Arabia, Bw. Suleiman Saleh, Jumanne Machi 29, 2016, amekaribishwa rasmi katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudi Arabia alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi Muhammad A. Tayeb, Mkurugenzi Mkuu wa Wizara hiyo.

Balozi Tayeb alimpokea Bw. Saleh Ofisini kwake Jeddah na kuahidi kutoa ushirikiano unaohitajika katika kuimarisha mahusiano baina ya Saudi Arabia na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuatia kusainiwa hivi karibuni Ikulu, Dar-es-Salaam, makubaliano ya mashirikiano baina ya nchi hizo mbili. Makubaliano hayo ambayo yalisainiwa na  Mhe. Adil Jubeir, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia na Mhe. Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yalishuhudiwa pia na Mhe. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top