Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Mbwana Samatta Aonja Machungu Kwa Mara ya Kwanza Kwenye Timu yake Mpya ya Genk..

Nyota wa Tanzania Mbwana Samatta na klabu yake ya Genk walitoka vichwa chini baada ya timu yao kuchapwa bao 2-1 na klabu ya Standard Liege kwenye mchezo wa ligi kuu ya Belgium uliochezwa usiku wa Jumamosi March 5.

Genk wakiwa ugenini ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 42 kipindi cha kwanza likifungwa na Nikolaos Karelis na kuipeleka Genk mapumziko ikiwa kifua mbele kwa bao 1-0.

Dakika tatu baada ya kipindi cha pili kuanza, Ivan Santini akaisawazishia Standard Liege kabla ya Jean-Luc Diarra Dompe kuifungia Standard bao la ushindi na kupeleka msiba kwa Genk.

Kama kawaida Samatta iliingia uwanjani dakika ya 81 kuchukua nafasi Karelis lakini bado haikutosha kubalili matokeo.

Samatta anaishuhudia klabu yake ya Genk ikipoteza kwa mara ya kwanza tangu ajiunge nayo mwezi January akitokea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemrasia Kongo.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top