Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Mwanafunzi Aliyeongoza Kitaifa Matokeo Kidato cha Nne Aahidiwa Ajira Na Benki ya CRDB

Benki  ya  CRDB  imemfungulia  Akaunti  ya  Scholarship  na  kumwekea  sh. Milioni 5  mwanafunzi  aliyefanya  vizuri  katika  mtihani  wa  kumaliza  kidato  cha nne  mwaka  2015,  Butogwa Shija  na  kumwahidi  ajira  pindi  amalizapo  masomo.

Hafla  hiyo  ilifanyika  jana  jijini  Dar  es  Salaam  ikiwa  ni  kuelekea   kilele  cha maadhimisho  ya  siku  ya  wanawake  duniani  leo, ambapo Butogwa  alipewa  zawadi  ili  kuwahamasisha  watoto  wa  kike  kwamba  wanaweza.

Pia  Mamlaka  ya  Elimu Tanzania (TEA)  ilimuongezea  mwanafunzi  huyo  kiasi  cha  shilingi 500,000  lengo  likiwa  ni  kuwahamasisha  watoto  wa  kike  ili  kuleta  haki  sawa  kwa  wote.

Naye Butogwa  aliahidi  kutumia  fursa  hiyo  vizuri  kwa  kusoma  kwa  bidii  bila  kubweteka  na  kuwataka  wanafunzi  wengine  kuweka  bidii  kwenye  masomo  yao.

Katika hatua  nyingine, Naibu Mkurugenzi Mtendaji  wa  CRDB, Esther Kitoka  alisema   wametoa  sh. milioni 20  zitakazosaidia  katika  ujenzi  wa  mabweni  kwa  watoto  wa  kike  ili  kuongeza  kasi ya  ufaulu  kwa  wanafunzi
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top